Tarehe
10 Septemba 2012 majaribio ya usafiri wa treni katika jiji la Dar es
salaam yalifanywa kuanzia Stesheni mpaka Ubungo Maziwa. Kufuatia
majaribio hayo kauli kuhusu changamoto zilizopo ilitolewa na Naibu
Waziri Dkt Charles Tizeba na maoni mbalimbali yametolewa na wadau
wengine kwenye vyombo vya habari tarehe 11 na 12 Septemba 2012.
Kwa nafasi yangu ya Mbunge wa Ubungo katika Jiji la Dar es salaam natambua kuwa majaribio hayo ni hatua muhimu katika suala ambalo tangu mwaka 2010 kwa nyakati mbalimbali nimeihoji Serikali kutaka utekelezaji wa haraka kwa kuzingatia kuwa suala hilo lilikuwa kwenye mipango zaidi ya miaka 10 iliyopita hata hivyo hatua zaidi na za haraka zinahitajika kwa huduma ya usafiri wa reli kuanza tarehe 1 Oktoba 2012 na kuweka mazingira bora ya usafiri huo kupunguza msongamano.
Kwa nafasi yangu ya Mbunge wa Ubungo katika Jiji la Dar es salaam natambua kuwa majaribio hayo ni hatua muhimu katika suala ambalo tangu mwaka 2010 kwa nyakati mbalimbali nimeihoji Serikali kutaka utekelezaji wa haraka kwa kuzingatia kuwa suala hilo lilikuwa kwenye mipango zaidi ya miaka 10 iliyopita hata hivyo hatua zaidi na za haraka zinahitajika kwa huduma ya usafiri wa reli kuanza tarehe 1 Oktoba 2012 na kuweka mazingira bora ya usafiri huo kupunguza msongamano.
Chanzo: Chadema
Post a Comment