Featured
    KWA HABARI NA MATANGAZO EMAIL : pbuyegu2@gmail.com ... Get a superior results by advertising with us by E- Mail us pbuyegu2@gmail.com We will bring Your Business to Light

    Featured Posts

Loading...

(TARPOA) inatarajia kufanya Mkutano wake wa kwanza Septemba 29 mwaka huu, Kurasini


Na Frank Geofray-Jeshi la Polisi.
 Chama cha Askari Wastaafu wa Jeshi la Polisi (TARPOA) kinatarajia kufanya Mkutano wake wa kwanza Septemba 29 mwaka huu katika Chuo cha Taaluma za Polisi Kurasini kwa lengo la kujadili mambo mbalimbali ikiwemo kulsaidia Jeshi la Polisi katika kukabiliana na uhalifu.
Hayo yalisemwa Mwenyekiti wa TARPOA, Kamishna Mstaafu wa Jeshi la Polisi Bw.Hilal Rashid wakati alipokuwa akizungumza na Waandishi wa Habari Jijini Dar es Salaam kuhusiana na mkutano huo ambao utawakutanisha wastaafu wote wa Jeshi la Polisi .
Kamishna Mstaafu Rashid alisema malengo ya kuanzisha Chama hicho nikuwaunganisha wastaafu wote wa Jeshi la Polisi na hatimaye kuwaendeleza katika nyanja mbalimbali ili waweze kuutumia uzoefu wao katika kuhakikisha amani na usalama vinadumu hapa Nchini.
Aidha alitoa wito kwa Askari wastaafu wote wa Jeshi la Polisi kujiunga katika Chama hicho kwakuwa kitawasaidia katika kupata maendeleo na kulisaidia Taifa kwa taaluma walizonazo.
Kwa Upande wake Msemaji wa Jeshi la Polisi Nchini,Mrakibu Msaidizi wa Polisi Bi. Advera Senso alisema Chama hicho ni muhimu sana kwa kuwa kitalisaidia Jeshi la Polisi hasa katika Dhana yake ya Polisi Jamii na Ulinzi Shirikishi kwakukizingatia wastaafu hao wanauzoefu katika nyanja ya ulinzi na usalama .
Bi Senso alisema wao kama Jeshi la Polisi watafanya kazi na TARPOA na watashirikiana nao kwa kuwa wanatambua mchango wao katika kipindi chote walicholitumikia Jeshi hilo mpaka hivi sasa.
Download Our App

Post a Comment

CodeNirvana

BLOG RAFIKI

© Copyright EMMANUEL SHILATU - BREAKING NEWS BLOG
Back To Top