WASANII sanaa za maonesho nchini wamepewa changamoto ya kutambua kuwa watalii ni hadhira ambayo wanaweza kuilenga katika ubunifu wa kazi zao ili kuweza kukuza utalii wa kiutamaduni ambao utasaidia kuongeza mapato kwa ajili ya maendeleo yao na taifa zima.
kauli
hiyo ilitolewa jana na Mkuu wa Taasisi ya Sanaa na Utamaduni(TAsuBA)
Juma Bakari wakati akiwalisisha mada ya ‘Sanaa za Maonesho kama Kivutio
cha Utalii Tanzania’ wakati wa kongamano la Tamasha la 31 la Sanaa na
Utamaduni lililofanyika kwenye uwanja wa taasisi hiyo iliyopo Bagamoyo
mkoani Pwani.
Alisema
sanaa za maonesho ni kivutio kikubwa cha cha utalii ni muhimu wasanii
kuwa na mtazamo huo ili kuangalia fursa zilizopo. Lazima watambue
watalii ni hadhira ambayo wanaweza kuwalenga kwa kuwafahamu kwa makundi.
Alitolea
mfano kuwa katika kipindi cha mwaka 2005 sekta ya utalii imeingiza
mapato makubwa na imekuwa chanzo cha mapato ya fedha za kigeni,ambapo
nchi yetu ilipata dola za Marekani bilioni 1.8 na inatarajia kupata
dola za Marekani bilioni tatu ifikapo mwaka 2015.
Aliongeza
kuwa ni vizuri wasanii hao wakajifunza kutoka kwa wenzao wa Kenya na
Uganda ambao wamefanikiwa kuhamasisha utalii huo kwa kutumia ngoma na
muziki wa asili.
Mkuu
huyo wa taasisi hiyo alisema Lugha ya Kiswahili inaweza kuwa ni kivutio
cha watalii ikiwa wasanii hao watatayarisha tamthilia za lugha kwa
maneno mepesi.
Akizungumzia
kuhusu changamoto zinazowakabili katika kukuza utalii huo, alisema
zaidi ya vikundi 4000 vilivyosajiliwa ,hakuna hata kimoja kinachoonyesha
kukuza utalii huo. Alizitaja changamoto nyingine kuwa ni ukosefu wa
elimu ya biashara na ujasiriamali hali inayosababisha vikundi vingi
kutegemea wafadhili hatimaye kuanzishwa halafu vinakuwa havipo.
Aidha
alifafanua kuwa kampuni za kitalii nazo zinachangia kutokuza utalii huo
kwa kuwa kwa mujibu wa takwimu za Wizara ya Maliasili za mwaka
2011-2012 kampuni hizo ziko 385, kati ya hizo 85 ni za kigeni . Pia
kulingana na utafiti uliofanywa hata zilizobakia zinaendeshwa na wageni
ambao sio jambo rahisi kwa wao kuukuza kwa vile hawaufahamu.


Post a Comment