Featured
    KWA HABARI NA MATANGAZO EMAIL : pbuyegu2@gmail.com ... Get a superior results by advertising with us by E- Mail us pbuyegu2@gmail.com We will bring Your Business to Light

    Featured Posts

Loading...

JAJI KIONGOZI AMWAPISHA KAMISHNA WA UTAWALA NA FEDHA WA MAGEREZA

 

DAR ES SALAAM, Tanzania

JAJI Kiongozi wa Mahakama Kuu nchini, Fakihi Jundu, amemuapisha Kamishna wa Utawala na Fedha wa Magereza, Gaston Sanga kuwa Mjumbe wa Tume ya Polisi na Magereza.

Akizungumza na wandishi wa habari baada kumuapisha Kamshna huyo, Jaji huyo alisema tume hiyo imeundawa kwa nujibu wa sheria za nchi kwa ajili ya kuteleleza majuku ya Idara hizo mbili, ambapo kazi yake ni kusimamia nidhamu ya maofisa wasaidizi
Jundu alisema kuapishwa kwa Kamishna huyo kunafuatia baada ya wenzake wawili kuwapishwa Oktoba Mwaka huu, huku yeye akiwa safarini Mkoani Mbeya.

“Mimi leo siyo msemaji jaribuni kuzungumza naye Kamishna kile mnachohitaji”alisema Jaji Jundu.

Naye Sanga alisema tahakikisha anafanya kazi kwa uwadilifu ili tume hiyo iweze kuaminika miongoni mwa maofisa wa Jeshi la Polisi na Magereza nchini.

Alisema Tume hiyo imeundwa mahususi kwa ajili ya kusimamia maslahi ya maofisa wa wa saidizi wa Idara hizo mbili ikiwa ni pamoja na kusimamia upandishwaji vyo wa maofisa hao.
Maofisa wengine wawili Magereza ambao ni pamoja na Gerali John Minja na Kamshna wa sheria aktika ofisi hiyo ya Magereza ,Juma Ally waliapishwa Otoba 30 mwaka huu.
Download Our App

Post a Comment

CodeNirvana

BLOG RAFIKI

© Copyright EMMANUEL SHILATU - BREAKING NEWS BLOG
Back To Top