Featured
    KWA HABARI NA MATANGAZO EMAIL : pbuyegu2@gmail.com ... Get a superior results by advertising with us by E- Mail us pbuyegu2@gmail.com We will bring Your Business to Light

    Featured Posts

Loading...

JARIBIO LA MAPINDUZI YA KIJESHI LAZIMWA NCHINI LIBYA.


http://kiswahili.irib.ir/media/k2/items/cache/96150a3351646aa118f66bad193da703_XL.jpg
DURU za habari kutoka Libya zinaripoti juu ya kuzimwa jaribio la
mapinduzi ya kijeshi yaliyopangwa na maafisa wa zamani wa jeshi la
nchi hiyo.
Taarifa zinasema kuwa, kundi la kwanza la maafisa hao tayari
limeshakamatwa katika mji wa Benghazi mashariki mwa nchi hiyo,
huku shirika la kijasusi la kijeshi la Libya likiendelea na msako wa
kuwatia mbaroni viongozi wengine wa mtandao huo huko Tripoli.

Hii ni mara ya kwanza kutokea jaribio la mapinduzi ya kijeshi nchini
Libya tokea alipong'olewa madarakani dikteta Kanali Muammar
Gaddafi.

Hivi karibuni kumetokea mauaji yanayofanywa na watu
wasiojulikana dhidi ya viongozi wa kisiasa na kijeshi nchini humo,
miongoni mwao wakiwemo AbdulFattah Younnis aliyekuwa
Kamanda wa Operesheni za kijeshi dhidi ya vikosi vya Gaddafi
katika kipindi cha vita vilivyotokea mwaka uliopita nchini humo,
na Kanali Faraj al Darsi Kamanda wa Usalama wa Benghazi.

Download Our App

Post a Comment

CodeNirvana

BLOG RAFIKI

© Copyright EMMANUEL SHILATU - BREAKING NEWS BLOG
Back To Top