Featured
    KWA HABARI NA MATANGAZO EMAIL : pbuyegu2@gmail.com ... Get a superior results by advertising with us by E- Mail us pbuyegu2@gmail.com We will bring Your Business to Light

    Featured Posts

Loading...

MSHINDI EBSS KUPATIKANA KESHO DIAMOND JUBILEE NA ATAZOA MILIONI 50

 


Mkurugenzi wa kampuni ya Benchmark Productions Limited, Ritha Poulsen akizungumza na Waandishi wa Habari mchana wa leo ukumbi wa Diamond Jubilee, Dar es Salaam kuhusu shindano Epiq Bongo Star Search 2012 (EBSS) litakalofanyika kesho kwenye ukumbi huo huo wa Diamond Jubilee, Dar es Salaam. Wengine kulia kwake na kushoto ni miongoni mwa washiriki wa shindano hilo walioingia fainali.


Mkurugenzi wa kampuni ya Benchmark Productions Limited, Ritha Poulsen akizungumza na Waandishi wa Habari mchana wa leo ukumbi wa Diamond Jubilee, Dar es Salaam kuhusu shindano Epiq Bongo Star Search 2012 (EBSS) litakalofanyika kesho kwenye ukumbi huo huo wa Diamond Jubilee, Dar es Salaam. Wengine kulia kwake na kushoto ni miongoni mwa washiriki wa shindano hilo walioingia fainali.

Washiriki wa EBSS Salma Yussuf Abushir, Nsami Nkwabi, NshomaNghangasamala, Walter Chilambo na Wababa Mtuka wakiwa na Ritha Poulsen. Je, nani ataondoka na kitita cha Sh. Milioni 50 kesho?
Na Bin Zubeiry
BAADA ya miezi mitatu ya mchuano mkali hatimaye mshindi wa shindano la kuimba la Epiq Bongo Star Search atapatikana leo katika fainali kali inayofanyika katika ukumbi wa Diamond Jubilee.
Mshindi atajinyakulia shilingi milioni hamsini pamoja na mkataba wa kurekodi kutoka kwa wadhamini pekee wa shindano hilo kampuni ya simu za mikononi ya Zantel.
Washiriki walioingia kwenye fainali hizo ni EBSS06: Nsami Nkwabi, EBSS07: Nshoma Ng’hangasamala, EBSS09: Salma Abushiri, EBSS11: Wababa Mtuka (Dar) na EBSS12: Walter Chilambo (Dar).
Wasanii watakaoburudisha ni Rich Mavoko, Omi Dimpoz, Ben Paul, Lina, Amini, Mzee Yusuf, Haji Ramadhan, Mwasiti, Ditto, Laila Rashid, Linex na Barnaba.
Akizungumzia fainali hizo, jaji mkuu wa shindano hilo, Madam Ritha Paulsen, aliwashukuru watanzania kwa ushirikiano waliowapa toka shindano limeanza mpaka leo wanahitimisha kwa fainali.
‘Kama mlivyoona shindano hili toka lilipoanza mwaka huu limekuwa la kimataifa zaidi, hivyo tarajieni fainali za kipekee na zitakazoweka rekodi kwenye tasnia ya burudani na ni matarajio yetu kwamba mshindi wa usiku huu atafanya vizuri kwenye muziki’ alisema Madam Ritha.
Kwa upande wake Afsa Biashara mkuu wa Zantel, bwana Sajid Khan alisisitiza utayari wa kampuni yake katika kuwaendeleza vijana wa kitanzania kufikia ndoto zao lakini aliomba pia wadau wengine wa sanaa kuwapa washirikiano washiriki wote.
‘Zantel, pamoja na kumpa mshindi zawadi ya milioni hamsini lakini pia tutampa mkataba wa kurekodi, na washiriki wengine watapewa nafasi ya kurekodi wimbo mmoja mmoja lakini juhudi hizi zitafanikiwa ikiwa tutapata ushirikiano wa kutosha kutoka kwa wadau’ alisema Khan.
Shindano hilo limekuwa likirushwa hewani na kituo cha runinga cha ITV, lilianza mwezi wa sita kwa kufanya usaili mikoani, ambalo mwaka huu lilienda mikoa nane-Mbeya, Dodoma, Mwanza, Tanga, Dar es Salaam, Zanzibar, Lindi pamoja na Arusha.
Kwa mara ya kwanza pia shindano hilo liliweza kufanya usaili kwa njia ya simu ili kuwapa nafasi vijana zaidi ambao hawakufikiwa na majaji.
Epiq Bongo Star Search ni kipindi cha televisheni ambacho huibua vipaji vya muziki kwa vijana wa kitanzania na kinatengenezwa na Benchmark Productions, na toka kimeanzishwa mwaka 2006 kimekuwa ni kipindi kinachotazamwa zaidi Afrika mashariki kwa kufikisha watu milioni 3 wanaotazama kwa kila kipindi.
Mwaka huu kinadhaminiwa na kampuni ya simu za mikononi ya Zantel, na mshindi atapata zawadi ya shilingi milioni 50 pamoja na mkataba wa kurekodi.
Download Our App

Post a Comment

CodeNirvana

BLOG RAFIKI

© Copyright EMMANUEL SHILATU - BREAKING NEWS BLOG
Back To Top