Featured
    KWA HABARI NA MATANGAZO EMAIL : pbuyegu2@gmail.com ... Get a superior results by advertising with us by E- Mail us pbuyegu2@gmail.com We will bring Your Business to Light

    Featured Posts

Loading...

ASKARI WAWILI WAFARIKI DUNIA KATIKA GHASIA KASKAZINI MWA NIGERIA.



Ramani ya jimbo la Bauchi, Nigeria
KUMETOKEA ghasia kadha kaskazini mwa Nigeria katika eneo la mbali kaskazini-mashariki mwa nchi, watu wanaoshukiwa kuwa wafuasi wa kundi la wapiganaji wa Kiislamu, Boko

Haram, walishambulia kanisa, kituo cha polisi, na ofisi za uhamiaji na ushuru katika mji wa Gamboru-Ngala, karibu na mpaka wa Cameroon.

Askari polisi wawili waliuwawa.

Pia kumetokea mapambano baina ya watu waliokuwa na silaha na askari wa usalama kwenye mji wa Azare, katika jimbo la Bauchi, kaskazini mashariki mwa nchi.

Wakaazi wa huko wanasema washambuliaji wawili waliuwawa na wa tatu amejificha ndani ya nyumba ambayo sasa imezingirwa na polisi.
Download Our App

Post a Comment

CodeNirvana

BLOG RAFIKI

© Copyright EMMANUEL SHILATU - BREAKING NEWS BLOG
Back To Top