Featured
    KWA HABARI NA MATANGAZO EMAIL : pbuyegu2@gmail.com ... Get a superior results by advertising with us by E- Mail us pbuyegu2@gmail.com We will bring Your Business to Light

    Featured Posts

Loading...

Mkapa ahimiza wahitimu vyuo vikuu kujiajiri

RAIS mstaafu wa awamu ya tatu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Benjamini Mkapa amewashauri wahitimu wa vyuo vikuu nchini kubuni ajira zitakazo waletea maendeleo ili kuweza kukabiliana na changamoto ya ajira inayosumbua nchi nyingi duniani.

Ushauri huo ameutoa juzi wakati wa mahafali ya tatu ya Chuo Kikuu cha Kumbukumbu ya Sebastiani Kolowa (Sekomu) yaliyofanyika katika ukumbi mpya chuoni hapo.

Mkapa alisema kuwa wahitimu wengi kutoka vyuo vikuu huangaika kutafuta ajira na kuwashauri ni vyema wakawa wakabunifu wa ajira zitakazowaletea faida na kuendeleza jamii inayowazunguka na hatimaye taifa zima.

Alisema nyakati hizi kunaupungufu mkubwa wa ajira na si Tanzania bali katika nchi nyingine nyingi duniani .

Mkapa alisisitiza kuwa wahitimu ambao watakosa ajira wajiunge kwenye vikundi vya taaluma zao ili waendelee kujifunza na kubuni mbinu za kujikwamua kwenye matatizo yatakayo wakabili katika maisha yao ya baadaye.

Wakati huo huo Mkuu wa Chuo hicho cha Sekomu , Dk Stephan
Munga aliitaka Serikali kutafuta njia mbadala za kuweza kupanua wigo wa ajira ili vijana wanaotoka vyuo vikuu waweze kupata ajira pindi wanapo hitimu masomo yao ya juu.

Kwa upande mwingine Munga aliwataka wahitimu kutumia vyema elimu walioipata kama silaha katika maisha yao ili wapate heshima kwa jamii.
Hata hivyo aliwataka wahitimu wawe na lugha ya kiungwana katika jamii na kwamba wasidharau wengine kwa kuwa wao tayari wana elimu ya juu.
Download Our App

Post a Comment

CodeNirvana

BLOG RAFIKI

© Copyright EMMANUEL SHILATU - BREAKING NEWS BLOG
Back To Top