Featured
    KWA HABARI NA MATANGAZO EMAIL : pbuyegu2@gmail.com ... Get a superior results by advertising with us by E- Mail us pbuyegu2@gmail.com We will bring Your Business to Light

    Featured Posts

Loading...

NGASSA SASA ANUNULIWA KWA MILIONI 240 NA EL MEREIKH

* Sasa anunuliwa kwa milioni 240 na kuweka rekodi 

* Simba, Azam zalamba Milioni 80 kila moja, Ngassa naye alamba mil 80 na mshahara mnono. 


 Klabu ya El Mereikh ya Sudan imetoa dola 100,000 (shs 160 million) kuzilipa klabu za Azam FC na Simba SC ili kuondoa mgogoro wa usajili wa mchezaji Mrisho Ngassa. 


 Awali El Mereikh ililipa Dola za Kimarekani 75,000 (shs million 120) kwa klabu ya Azam FC pekee kwa ajili ya usajili wa mchezaji huyo na kuzua mtafauku mkubwa dhidi ya klabu ya Simba na kuamua kuweka pingamizi katika Shirikisho la Kandanda nchini (TFF), CAF na Fifa. 


 Simba ilidai kuwa Ngassa ni mchezaji wao halali kutokana na ukweli kuwa ilimnunua kwa shs milioni 25 zilizotakiwa na Azam FC na kumlipa stahiki zake zote kwa mujibu wa mkataba huo. 


 Pamoja na kupata upinzani mkubwa kutoka kwa timu ya Azam FC kutokana na ukweli kuwa Ngassa alikuwa akiichezea Simba kwa mkopo, Simba iling’ang’ania na msimamo wake na kupeleka suala hilo mbele ya vyombo vya sheria vya TFF ili kupata haki yake.


 TFF ilishauri klabu hizo kukaa meza meza moja ili kuona kuwa wanaondoa utata huo, jambo ambalo lilifanyika Jumatatu na Jumanne na kufikia muafaka huo na El Mereikh kulipa fedha zaidi na kumfanya mchezaji huyo kusajiliwa kwa Dola za Kimarekani 150,000 (Milioni 240 ukijumuishs Dola za Kimarekani 50,000 atakazolipwa Ngassa na El Mereikh) na kuwa mchezaji wa kwanza kusajiliwa kwa kitita hicho hapa nchini. 


 Katibu Mkuu wa Simba, Evodius Mtawala alisema kuwa wamefarijika sana na makubaliano hayo na wao kutoa kipingamizi cha Ngassa kwenda kufanyiwa vipimo vya afya mjini Khartoum kabla ya kusaini mkataba wa kuichezea timu hiyo. 


 Mtawala alisema kuwa hayo ni matunda ya kujadili mambo katika meza moja na wala si kwa kutimia vyombo vya habari kwani wao walijua haki yao ipo wapi. Afisa Habari wa Azam FC, Jaffer Idd alithibitisha makubaliano hayo na kusema uongozi wa klabu hiyo chini ya makamu mwenyekiti, Shan Christoms na Twalib Suleiman aliyemwakilisha katibu mkuu, Nassoro Idrissa ndiyo waliofikia makubaliano hayo. 


 Simba SC iliwakilishwa na Mtawala na Makamu Mwenyekiti, Geofrey Nyange Kaburu aarufu kwa jina la Perez.“Ni faraja kwetu kufikia maamuzi haya, lengo ni kumfanya Ngassa atomize ndoto yake katika soka na wala si vinginevyo,” alisema Idd
Download Our App

Post a Comment

CodeNirvana

BLOG RAFIKI

© Copyright EMMANUEL SHILATU - BREAKING NEWS BLOG
Back To Top