Featured
    KWA HABARI NA MATANGAZO EMAIL : pbuyegu2@gmail.com ... Get a superior results by advertising with us by E- Mail us pbuyegu2@gmail.com We will bring Your Business to Light

    Featured Posts

Loading...

SERIKALI KUWAKAMATA WALIOANZISHA VIWANDA BUBU VINAVYOZALISHA BIDHAA CHINI YA KIWANGO

NAIBU Waziri wa Viwanda na Biashara, Gregory Teu, amesema serikali kuanzia sasa itawakamata baadhi ya watu waliyojianzishia viwanda bubu vinavyozalisha bidhaa hafifu nchini.

Kauli hiyo ilitolewa, na waziri huyo wakati alipotembelea viwanda vinavyomilikiwa na Kampuni ya MMI Steel Mills Limited vilivyoko Mikocheni jijini Dar es Salaam jana.
Alisema lengo la kuwakamata watu hao ambao wamo hata wageni , na kuwafikisha kwenye vyombo vya sheria ni kudhibiti bidhaa hizo kwenye soko ambapo zimekuwa zikiwatia hasara wananchi pia kuviharibia sifa baadhi ya viwanda.
Teu alisema viwanda hivyo vimekuwa vikiiga bidhaa kama nondo na mbati, kutumia nembo za kampuni mbalimbali zinazotambulika nchini kama vile MMI Steel Mills Limited.
Alisema kutokana na ubabaishaji huo unaofanywa na baadhi ya watu, serikali itahakikisha inazisaidia kampuni zote zilizoanzishwa kwa kufuata sheria.
“Kampuni hii ya MMI Steel Mills imekuwa kwa muda mrefu ikitoa mchango mkubwa katika kuchangia pato la taifa haswa kwenye eneo la kodi pia imepanua wigo wa ajira kwa Watanzania ambapo pia kimekuwa kikiingizia Tanesco jumla ya sh. bilioni 1 kama bili kwa mwezi ”alisema Teu.
Akizungumzia kuingiliana kwa mipaka kati ya Kiwanda hicho na Shirika la Maendeleo ya Taifa (NDC katika mradi wa kutengeneza chuma cha Liganga na mkaa wa mawe huko Katewaka, Teu alisema, hata yeye utata huo umemshtua sana.
Alisema matatizo hayo yamesababishwa utoaji wa zabuni, kutokana na upande mmoja kutokuwa makini ambapo pia aliwaomba wasichoke, watalifanyia kazi kama wizara.
Awali Mhandisi, Raulence Manyama viwanda hivyo vya chuma, vilikuwa vikikabiliwa na changamoto ya upatikanaji wa chuma.
Alisema hadi kufikia mwa 2012 kulikuwa na viwanda na viwanda 21 vya chuma nchini vyenye uwezo wa kuzalisha zaidi ya tani 200,000 za chuma kwa mwaka.
Aliasa serikali kuongeza uwezo nchi kuzalisha aina nyingi ya bidhaa ya chuma ambazo kwa sasa zinatoka nchi za nje, hizo ni hot-roll coils, cold coils, flat bars na aina nyingi za chuma.
Download Our App

Post a Comment

CodeNirvana

BLOG RAFIKI

© Copyright EMMANUEL SHILATU - BREAKING NEWS BLOG
Back To Top