Featured
    KWA HABARI NA MATANGAZO EMAIL : pbuyegu2@gmail.com ... Get a superior results by advertising with us by E- Mail us pbuyegu2@gmail.com We will bring Your Business to Light

    Featured Posts

Loading...

TIMU YA BUNGE SPORTS CLUB YA TANZANIA YAIKANDAMIZA BUNGE YA KENYA MAGOLI 5-0

 

Tanzania Bunge Sports Club Football imefanya maajabu katika uwanja wa Nyayo jijini Nairobi jana kwa kuwabamizwa wenyeji wao timu ya Kenya Bunge Sports Club Football mabao 5 kwa nunge katika michezo ya mabunge ya nchi za Jumuiya ya Afrika Mashariki yanayoendelea jijini Nairobi. Mashindano hayo yaliyofunguliwa rasmi juzi tarehe 7 Disemba na Spika wa Bunge la Afrika Mashariki Mh. Margreth Natongo Zziwa akisisitiza “let the best team win” tayari yamezikutanisha timu ya Bunge la Uganda na timu ya Jumuiya ya Afrika Mashariki ambapo timu hizo zimetoka sare ya
Wakati wa kuhitimisha karamu ya mabao kwa timu ya Kenya, Watanzania walijikuta uwanjani peke yao wakishangilia huku mashabiki-wenyeji wakiwa wameondoka uwanjani hapo. leo Tanzania itapambana na Rwanda kwenye mpira wa miguu katika uwanja wa City Stadium, na Wabunge wanawake watakutana na Kenya kwenye mpira wa kikapu Nyayo Stadium. Mashindano haya yanalenga kuimarisha ushirikiano na kuitangaza zaidi Jum uiya ya Afrika Mashariki.
Katika mashindano haya ambayo hufanyika kila mwaka huyakutanisha mabunge ya nchi za Tanzania, Kenya, Uganda, Burundi na Rwanda. Waratibu wa michezo hii ni Jumuiya pamoja na Bunge la Afrika Mashariki. Kwa mwaka huu Burundi haikushiriki.
Chini ya ukufunzi wa Naibu Waziri (TAMISEMI) Mhe. Kasim Majaliwa (Mb) .na uongozi wa Mhe. Idd Azzan (Mb) mabao hayo yalifungwa na Mhe Amos Makala (Mb), Yusuf Soka (2), Mark Tanda na Mhe. Joshua Nassari. (Na Prosper Minja)
Download Our App

Post a Comment

CodeNirvana

BLOG RAFIKI

© Copyright EMMANUEL SHILATU - BREAKING NEWS BLOG
Back To Top