Featured
    KWA HABARI NA MATANGAZO EMAIL : pbuyegu2@gmail.com ... Get a superior results by advertising with us by E- Mail us pbuyegu2@gmail.com We will bring Your Business to Light

    Featured Posts

Loading...

UGONJWA WA JAJI WAKWAMISHA USIKILIZWAJI WA RUFAA ILIYOKATWA NA DPP-DK.ELEZER FELESHI KUPINGA HUKUMU YA KESI YA MAUJI YA WATU WANNE DHIDI YA ACP ABDALLAH ZOMBE LEO JIJINI DAR ES SALAAM


 

Mwadishi Mashuhuri wa Makala mbalimbali na habari za Kimahakama Happiness Katabazi(Kulia)akiwa na 'mkwe wake 'ACP-Abdallah Zombe leo asubuhi katika Mahakama ya Rufaa Dar es Salaam, muda mfupi baada ya rufaa iliyokatwa na DPP-Dk.Elezer Feleshi kupinga hukumu ya kesi ya mauaji ya watu wanne dhidi ya Zombe na wenzake kushindwa kusikilizwa na mahakama hiyo kwasababu jaji mmoja kati ya majaji watatu wanaosilikiza kesi hiyo anaumwa.
Wakili Mwandamizi wa Serikali Angaza Mwipopo akisalimiana ACP-Abdallah Zombe leo asuhubi ndani ya Mahakama ya Rufaa
Hii ndiyo timu ya mawakili waandamizi wa serikali katika rufaa ya Zombe Timoth Vitalis, Edwin Kakolaki,Angaza Mwipopo,Prudence Rweyongeza,Alexander Mzikilia,Mgaya Mtaki na Peter Njike, wakiwa ndani ya ukumbi wa mahakama ya rufaa Dar es Salaam, lakini hata hivyo rufaa hiyo haikuweza kusikilizwa kwasababu jaji mmoja anayeunda jopo la majaji wa tatu anaumwa.
Zombe na wakili wake Richard Rweyongeza.Na upande wa jamhuri unawakilishwa na timu ya mawakili waandamizi wa serikali saba.Picha na Happiness Katabazi
--
Na Happiness Katabazi

MAHAKAMA ya Rufaa Dar es Salaam, jana ilishindwa kuanza kusikiliza rufaa iliyokatwa na Mkurugenzi wa Mashtaka(DPP), Dk.Eliezer Feleshi dhidi ya aliyekuwa M kuu wa Upelelezi wa Jeshi la Polisi(ACP),Abdallah Zombe na wenzake kwasababu jaji mmoja ambaye anaunda jopo la majaji wa tatu Semistocles Kaijage anaumwa.

DPP.Feleshi anapinga hukumu iliyotolewa na Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam na Jaji Salum Massati ambaye kwasasa ni jaji wa mahakama ya rufaa kwasababu hukumu ile ina makosa ya kisheria na kwamba jaji Masati akupaswa kuwaachilia huru wajibu rufaa hao na Jaji Natalia Kimaro ndiyo aliarisha rufaa hiyo leo asubuhi na kuzieleza pande zote mbili kuwa tarehe ya kuja kusikilizwa rufaa hiyo watapatiwa kwa maandishi.
Download Our App

Post a Comment

CodeNirvana

BLOG RAFIKI

© Copyright EMMANUEL SHILATU - BREAKING NEWS BLOG
Back To Top