SHIRIKISHO la soka nchini
TFF limesema kuwa litafanya majadiliano na vilabu vya SIMBA na YANGA ambavyo
vimetishia kutowaruhusu wachezaji wake kujiunga na kambi ya TAIFA STARS
iliyopangwa kuanza JANUARI SITA mwaka huu.
Msemaji wa
shirikisho hilo , BONIFACE WAMBURA amesema kambi hiyo ya TAIFA STARS dharura ni
ya wiki mbili ambayo itamsaidia kocha KIM PAULSEN kuwafahamu vizuri wachezaji
ambao amewaita kutoka katika timu ya KILIMANJARO STARS na wale wa ZANZIBAR
HEROES (PAUSE)
Kuwaita wachezaji wa TAIFA STARS ni kutokana
na kocha PAULSEN kuanza kufanya matayarisho ya kuikabili vizuri timu ya MOROCCO
katika mashindano ya kutafuta kombe la dunia mchezo utakaochezwa mwezi Machi
mwaka huu.
Katika kundi la TAIFA STARS kuna timu
nyingine za IVORY COAST na GAMBIA.
Katika hatua nyingine , msemaji wa TFF ,
BONIFACE WAMBURA amesema bado michezo ya kirafiki inatafutwa ili kuiandaa TAIFA
STARS na mashindano hayo.
SHIRIKISHO la soka nchini
TFF limesema kuwa litafanya majadiliano na vilabu vya SIMBA na YANGA ambavyo
vimetishia kutowaruhusu wachezaji wake kujiunga na kambi ya TAIFA STARS
iliyopangwa kuanza JANUARI SITA mwaka huu.
Msemaji wa
shirikisho hilo , BONIFACE WAMBURA amesema kambi hiyo ya TAIFA STARS dharura ni
ya wiki mbili ambayo itamsaidia kocha KIM PAULSEN kuwafahamu vizuri wachezaji
ambao amewaita kutoka katika timu ya KILIMANJARO STARS na wale wa ZANZIBAR
HEROES (PAUSE)
Kuwaita wachezaji wa TAIFA STARS ni kutokana
na kocha PAULSEN kuanza kufanya matayarisho ya kuikabili vizuri timu ya MOROCCO
katika mashindano ya kutafuta kombe la dunia mchezo utakaochezwa mwezi Machi
mwaka huu.
Katika kundi la TAIFA STARS kuna timu
nyingine za IVORY COAST na GAMBIA.
Katika hatua nyingine , msemaji wa TFF ,
BONIFACE WAMBURA amesema bado michezo ya kirafiki inatafutwa ili kuiandaa TAIFA
STARS na mashindano hayo.
Post a Comment