Featured
    KWA HABARI NA MATANGAZO EMAIL : pbuyegu2@gmail.com ... Get a superior results by advertising with us by E- Mail us pbuyegu2@gmail.com We will bring Your Business to Light

    Featured Posts

Loading...

YANGA KUFANYA MKUTANO WAO HII LEO


KLABU ya Yanga chini ya Mwenyekiti wake, Yusuf Manji, leo inafanya mkutano mkuu wa kawaida kwenye Ukumbi wa Bwalo la Maofisa wa Jeshi, Oysterbay, jijini Dar es Salaam.

Mkutano huo ambao ni wa kwanza kwa uongozi wa Manji uliochaguliwa Julai 15, mwaka jana, utajadili mambo mbalimbali ya maendeleo ya klabu hiyo kongwe nchini.

Awali, mkutano huo ulikuwa ufanyike Desemba 8, mwaka jana, lakini ukasogezwa kupisha sherehe za miaka 51 ya uhuru ambapo kilele chake kilifanyika Desemba 9.

Kwa mujibu wa Katibu Mkuu wa klabu hiyo, Lawrance Mwalusako, maandalizi kwa ajili ya mkutano huo utakaoanza saa mbili asubuhi yamekamilika ambapo amewaomba wanachama kujitokeza kwa wingi kujadili mipango mbalimbali ya maendeleo.

“Huo ni mkutano wa wanachama hivyo kutajadiliwa masuala mengi ambayo yatajitokeza hukohuko kwenye mkutano, tunawaomba wana-Yanga kujitokeza kwa wingi,” alisema.
Download Our App

Post a Comment

CodeNirvana

BLOG RAFIKI

© Copyright EMMANUEL SHILATU - BREAKING NEWS BLOG
Back To Top