Featured
    KWA HABARI NA MATANGAZO EMAIL : pbuyegu2@gmail.com ... Get a superior results by advertising with us by E- Mail us pbuyegu2@gmail.com We will bring Your Business to Light

    Featured Posts

Loading...

MWANAFUNZI UDSM AJINYONGA HADI KUFA .... HII HAPA STORY KAMILI

 





.
Mwanafunzi wa kiume wa mwaka wa pili sheria mwenye umri kati ya 22 mpaka 25 amejinyonga march 25 2013 pembeni ya madarasa chuo kikuu cha Dar es salaam ambapo saa nne asubuhi mwili wake ndio ulikutwa ukiwa unaning’inia kwenye mti, kwenye barua aliyoacha ameandika asilaumiwe mtu.

.
Hizi picha zimepigwa kwa simu.



Mwanafunzi wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM) mwaka wa pili Kitivo cha Sheria, Joseph Bernadina (25), amejinyonga kwa kutumia kamba na kukutwa ameifunga juu ya mti, katika eneo la Yombo chuoni hapo.




Makamu Mkuu wa Chuo hicho, Utawala, Profesa Yunus Mgaya, alithibitisha kutokea kwa tukio hilo na kwamba alipata taarifa hizo jana asubuhi.Aliongeza kuwa Jumamosi iliyopita alipokea simu kutoka kituo cha polisi cchuo hicho akielezwa kuwa kuna mwanafunzi alitishia kujiua, lakini aliwahishwa hospitali na kupatiwa ushauri kutoka kitengo maalum cha washauri wa chuoni hapo na kuruhusiwa Jumapili.




“Nilikuja tena kushituka leo asubuhi napokea simu kutoka kwa mshauri wa wanafunzi kuwa kuna wanausalama wamemkuta mwanafunzi akiwa amejinyonga juu ya mti huku akiwa na karatasi kwenye mfuko wa sharti ikimtambulisha pamoja na ujumbe uliosema, kifo chake kisihusishwe na mtu yeyote kwani amejiua kwa ridhaa yake --asisumbuliwe mtu yeyote kwani nimefanya hivi kwa maamuzi yangu mwenyewe pia nizikwe kwetu--” alisema.

Download Our App

Post a Comment

CodeNirvana

BLOG RAFIKI

© Copyright EMMANUEL SHILATU - BREAKING NEWS BLOG
Back To Top