.
Mkurugenzi Mkuu Nehemia Mchechu amesema kwa kawaida shirika la nyumba limekua likiingia ubia na watu binafsi wenye uwezo wa kujenga nyumba kama hizo ambapo liliingia ubia na kampuni ya ujenzi ya RAZA na kusaini mkataba wa kujenga jengo lenye gorofa 10 tu kwenye eneo hilo ingawa baadae kampuni hiyo iliomba kubadili mkataba ili wajenge gorofa 16.
Kuhusu umiliki kwa asilimia 25 kwenye jengo lililoporomoka, Mchechu amesema kwa ubia uliokuwepo walipaswa kupewa asilimia hizo baada ya ujenzi kukamilika na asilimia nyingine 25 wangepewa miaka kumi baadae kulingana na mkataba na hawakupaswa kuhusika kwenye gharama zozote wala taratibu za ujenzi.
.
Kwenye line nyingine, NHC imeunda timu kwa ajili ya kufanya ukaguzi katika miradi yake yote ya ujenzi wa ubia ili kujihakikishia usalama wa majengo husika.


Post a Comment