Featured
    KWA HABARI NA MATANGAZO EMAIL : pbuyegu2@gmail.com ... Get a superior results by advertising with us by E- Mail us pbuyegu2@gmail.com We will bring Your Business to Light

    Featured Posts

Loading...

Bonde la maji la Pangani lachukua sampuli ya maji Mto Karanga

 

Mtaalamu wa mazingira wa ofisi ya bonde la maji la Pangani ,Mhandisi Arafa Maggidi akiwa na mtaalamu wa vipimo kutoka kituo cha utafiti wa kuondoa Frolide cha Ngurdoto Godfrey Mkongo wakiangalia maji yanayodaiwa kuwa na kemikali yakiingia mto Karanga .
Mtaalamu wa mazingira wa ofisi ya bonde la maji la Pangani ,Mhandisi Arafa Maggidi akiwa na mtaalamu wa vipimo kutoka kituo cha utafiti wa kuondoa Frolide cha Ngurdoto Godfrey Mkongo wakichukua sampuli ya maji ya Mto Karanga kwa ajili ya vipimo.
Mwananfunzi wa chuo cha maabara ya sayansi,ufundi na teknolojia Arusha Stephew Msalale akichukua maji ya mto Karanga kama sampuli kwa ajili ya vipimo.
Mtaalamu wa mazingira wa ofisi ya bonde la maji la Pangani ,Mhandisi Arafa Maggidi akiwa na mtaalamu wa vipimo kutoka kituo cha utafiti wa kuondoa Frolide cha Ngurdoto Godfrey Mkongo wakichukua sampuli ya maji ya Mto Karanga kwa ajili ya vipimo.

Na Dixon Busagaga waglobu ya jamii Moshi

KUFUATIA kutolewa kwa taarifa za kutiririshwa kwa maji yanayodaiwa kuchanganyika na kemikali kutoka kwa baadhi ya viwanda vilivyoko kando ya mto Karanga ofisi ya Bonde la Pangani(PBWO) imelazimika kuchukua sampuli ya maji hayo kwa ajili ya kuyafanyia vipimo.

Hatua hiyo imekuja siku chache baada ya taarifa za kichunguzi zilizofanywa na Globu ya jamii baada ya kuwezeshwa na na mfuko wa waandishi wa habari(TMF) na kuripoti jinsi wakazi wa vijiji vya Chekeereni,Weruweru,Mijongweni na Kiyungi walivyo athirika na maji hayo.

Wataalamu wa vipimo vya maji Godfrey Mkongo na Steven Msalale mwanafunzi wa mwaka wa pili wa chuo cha ufundi,maabara ya sayansi na teknolojia wakiwa wameambatana na mtaalamu wa mazingira kutoka Bonde la maji la Pangani walifika katika mto huo kuchukua vipimo.

Jumla ya sampuli saba zilichukuliwa kutoka katika maeneo matatu tofauti ambayo yanadaiwa maji yake kuwa na madhara yanayo sababisha magonjwa mbalimbali kwa wakazi wa vijiji hivyo vilivyoko wilaya ya Moshi vijijini.

Maeneo ambayo maji yake yalichukuliwa sampuli ni pamoja na kabla na baada ya daraja la Bonite ambako kunafanyika shughuli za uoshaji wa Karoti kutoka katika mashamba yaliyoko Weruweru kabla ya kusafirishwa kupelekwa kwenye masoko ya ndani na nje ya mkoa wa Kilimanjaro.

Kwingine kulikochukuliwa sampuli ya maji ni eneo la daraja la gari Moshi ambako kuna maingilio makubwa ya maji ambayo yanatiririka kutoka katika viwanda vya Kibo paper na China paper yanayodaiwa kuwa na kemikali .

Sampuli ya maji iliyochukuliwa katika eneo hilo ni ile ya maji yatokayo katika maingilio ya kwainda cha Kibo Paper peke yake ,kasha ikachuliwa pia sampuli ya maji yatokayo katika maingilio ya kiwanda cha China paper.

Maeneo mengine ambayo maji yake yalichukuliwa sampuli ni pamoja na mbele ya daraja la gari Moshi eneo ambalo wananchi wengi wamekuwa wakifanya shughuli za kuoga kuosha vyombo pamoja na kufua nguo.

Eneo la mwisho ambako maji yake yalichukuliwa sampuli ni eneo kilipo kiwanda cha viberiti cha Kibo(Kibo match) ambacho pia yapo madai kuwa kiwanda hicho licha ya kuwa na eneo maalumu la kuhifadhia maji yake huenda yakawa yanapita chini ya ardhi.

Sampuli hizo zote zilipelekwa kituo cha utafiti wa viuatilifu nchini (TPRI) kilichopo jijini Arusha ambako mbali na vipimo vya kemikali zilizoko ndani ya sampuli hizo pia kulifanyika vipimo vya kujua endapo maji hayo yana bacteria wanao sababisha magonjwa mbalimbali kwa binadamu.

Akizungumzia zoezi hilo mtaalamu wa mazingira ofisi ya Bonde la maji la Pangani Arafa Maggidi alisema vipimo vingine vilipelekwa kituo cha utafiti wa kuondoa Frolide iliyopo Ngurdoto na vingine maabara kuu ya maji iliyopo Dar es salaam.

Alisema hadi sasa majibu ya vipimo hivyo kutoka katika maabara zote tatu hayajarejeshwa hali inayochangia hadi sasa ofisi hiyo kuendelea kuchukua hatua zaidi katika mto huo ili kuokoa wakazi wa maeneo ya vijiji vya Chekereni,Weruweru,Mijongweni na Kiyungi wanaoendelea kuyatumia maji hayo hadi sasa.
Download Our App

Post a Comment

CodeNirvana

BLOG RAFIKI

© Copyright EMMANUEL SHILATU - BREAKING NEWS BLOG
Back To Top