Meneja
Uhusiano wa Kituo cha Uwekezaji Tanzania (TIC) Pendo Gondwe akiwaelezea
waandishi wa habari juu ya mafanikio ya kuhamasisha uwekezaji kwa
wawekezaji wa ndani kwa kipindi cha kuanzia Januari 2012 mpaka desemba
2012 katika ukumbi wa Idara ya Habari, kushoto ni Mkurugenzi Msaidizi
Idara ya Habari Zamaradi kawawa na kulia ni Meneja Huduma Revocatus
Arbogast.
(PICHA NA ELIPHACE MARWA)
………………………………………………………
Kituo
cha Uwekezaji Tanzania TIC kinapenda kutoa taarifa kwa Umma kuhusu
mafanikio ya kuhamasisha uwekezaji kwa wawekezaji wa ndani kwa kipindi
cha kuanzia Januari 2012 mpaka Decemba 2012.
Kituo
cha Uwekezaji Tanzania (TIC) ni moja Taasisi ya Serikali ilianzishwa
chini ya Sheria ya Uwekezaji Tanzania, Namba 26 ya mwaka 1997 kwa
kuendeleza, kuratibu na kuwezesha uwekezaji katika Tanzania. Kama sehemu
ya jukumu letu, TIC ina jukumu la kuhamasisha uwekezaji na masuala
yanayohusiana na Uwekezaji kwa Watanzania ili Uwekezaji uweze kuwa na
manufaa kwa Watanzania kwa ujumla.
Katika
kipindi cha mwaka Januari 2012 mpaka Desemba Watanzania wameweza
kutambua umuhimu wa kuwekeza na wameweza kuchangamkia fursa katika sekta
mbalimbali. Katika kipindi hicho zaidi ya miradi 869 iliweza kusajiliwa
miradi ambayo inategemea kuzalisha kazi zaidi ya 174,412 yenye thamani
ya mitaji ya dola 11,420 milioni. Namba ya miradi hii ni kubwa kuwahi
kusajiliwa na Kituo.
Miradi
ya watanzanzia iliweza kuongoza kwa kwa TIC kusajili miradi 469 ya
wazawa ambayo ni asilimia 54% ya miradi yote iliyoweza kusajiliwa.
Sekta
tano zilizoongoza katika kusajiliwa ni sekta ya Utalii, Usafirishaji,
Uzalishaji viwandani , majengo ya biashara na kilimo. Sekta ya utalii
iliongoza kwa kusajili miradi 144, Usafirishaji miradi 92, Uzalishaji
viwandaji miradi 86, majengo ya biashara miradi 78 na kilimo miradi 28.
Katika
usajili wa miradi hiyo wawekezaji wa nje waliweza kusajiri miradi 205
ambayo ni asilimia 23.5, kiwango ambacho ni chini ya nusu ya kiwango cha
usajili wa miradi ya wawekezaji wa ndani. Miradi ya Ubia kati ya wageni
na watanzania ilikuwa ni 195 ambayo ni asilimia 22.5.
TIC
katika jitihada zake za kuongeza faida za uwekezaji katika uchumi wa
Tanzania pia walifanya shughuli kuu ikiwa ni pamoja na kuwawezesha
wawekezaji kupata vibali vyote vinavyohitajika chini ya One Stop Shop na
utoaji wa huduma kwa wawekezaji aftercare.
Post a Comment