Umoja
wa Vijana wa Chama cha Mapinduzi UVCCM umeamua kutumia wazee wa Chama
dhidi ya wanasiasa wanaopotosha na kutaka kutikisa misingi ya Mapinduzi
na Muuungano wa Tanganyika na Zanzibar .
Akitoa
taarifa kwa waandishi wa habari huko Makao Makuu ya CCM Kisiwanduwi
Naibu Katibu Mkuu wa Umoja wa Vijana UVCCM Shaka Hamdu Shaka amesema
watatumia wazee hao, wanaowaita silaha nzito, katika kukabiliana na
maadui na mashetani wanaotaka kutishia ustawi wa amani, utulivu na Umoja
wa Kitaifa.
Amesema
kuwa katika kuyaimarisha Mapinduzi na Muungano vijana hao wameamua
kuwatumia wazee ili kusafisha hali ya hewa inayochafuliwa na wapinga
umoja na mshikamano.
Amewataja
miongoni mwa wazee hao ni pamoja na Rais mstaafuu, Komandoo Dk Salmin
Amour Juma, Mzee Hamid Ameir Ali, Mzee Ibrahim Amani, Abdulrazaq Simai
Kwacha, Mzee Ali Khamis Jaribu na Mzee Ali Ameir.
“Tumedhamiria
kufanya kazi bega kwa bega na viongzi hao wakisimama upande wa
UVCCM katika kukiamsha na kukielezea kizazi kipya wapi tulikotoka,
mahali tulipo sasa na kule tunakoelekea”.alieleza Naibu katibu Shaka.
Aidha
alifahamisha kuwa viongozi hao watawatanguliza mstari wa mbele katika
mikutano yote ya UVCCM ili kuamsha ari ya kufanikisha mapambano dhidi
ya wale wanataka kuvunja umoja na mshikamano uliopo.
“UVCCM
hatukubali kuona mafanikio yaliyopatikana chini ya serikali ya Umoja wa
Kitaifa Zanzibar yanavurugwa na Viongozi wachache wenye hulka ya na
tama namaslahi yao binafsi”, alisisitiza nd. Shaka
Akizungumzia
uchumi, Katibu huyo amesema kuwa utalii ni nguzo kuu inayojenga uchumi
wa Zanzibar ambao unachangia asilimia 25 katika pato la Taifa na
kufanikiwa kwake linahitaji kuwepo na mazingira ya utulivu na amani.
Amesema
UVCCM inalaani vikali kwa kujitokeza maneno ya ubaguzi dhidi ya Upemba,
Uunguja na Ubara kwa kisingizio cha mjadala wa uundwaji wa katiba mpya
na kuwataka wananchi kuendelea kuishi kwa maelewano, umoja na kudumisha
mshikamano nchini.
Ameeeleza
kuwa UVCCM imejipanga kuzifufua maskani za CCM, kuimarisha mashina na
vijana katika nyanja za kisiasa, kiuchumi na kijamii.
Aidha
amewataka wananchi wapewe nafasi ya kutoa maoni yao katika mchakato wa
katiba unaoendelea badala ya kujitokeza mamluki wachache kutaka
kuwasemea wazanzibari
“Katiba
ni matakwa ya wananchi hivyo waachiwe watowe maoni yao bila ya
shindikizo na kushawishiwa na kundi au chama chochote cha siasa”,
alielzea katibu huyo.
IMETOLEWA NA IDARA YA HABARI MAELEZO ZANZIBAR
Post a Comment