Featured
    KWA HABARI NA MATANGAZO EMAIL : pbuyegu2@gmail.com ... Get a superior results by advertising with us by E- Mail us pbuyegu2@gmail.com We will bring Your Business to Light

    Featured Posts

Loading...

RAIS WA ZANZIBAR DK ALI MOHAMMED SHEIN AZINDUA GATI MPYA YA MALINDI ILIYOJENGWA NA BILIONEA BAKHRESA

 


IMEWEKWA JULAI 8, 2013 SAA 6:00 MCHANA

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Visiwani humo, Dk. Ali Mohammed Sheikn akizundua jiwe la Msingi la Gati mpya ya Malindi, Zanzibar asubuhi ya leo. Nyuma yake ni mmiliki wa makampuni ya S.S.B., Alhaj Sheikh Said Salim Awadh Bakhresa, ambaye amejenga Gati hiyo kwa ajili ya matumizi ya boti zake za Azam Marine na nyingine zote zinazofanya safari kati ya Dar es Salaam na Zanzibar na Zanzibar na Pemba.

Uzinduzi

Dk. Shein akisalimiana na Mzee Bakhresa alipowasili eneo la Gati hiyo ya kisasa

Hapa sasa safi kabisa; Mzee Bakhresa akimuongoza Dk. Shein kujionea sehemu mbalimbali za Gati hiyo

Mzee umefanya jambo kubwa na la heri; Dk. Sheik akizungumza na Mzee Bakhresa katika meza kuu wakati sherehe za uzinduzi wa Gati hiyo

Anamwaga wino; Dk. Shein akisaini kitabu cha wageni wa Azam Marine pembeni ya Mzee Bakhresa

Kwenda chini; Mzee Bakhresa akimuelekeza jambo Dk. Shein na msafara wake wakati akikagua gati hiyo

Twende kule ukaone zaidi; Mzee Bakhresa akimuongoza Dk. Shein

Si unaona mwenyewe; Mzee Bakhresa akimuelekeza kitu Dk. Shein

Tuanzie kule; Mzee Bakhresa na Dk Shein

Nimekubali Mzee; Dk Shein akijionea uzuri wa Gati mpya...Mzee Bakhresa kulia

Watoto hawa walitoa burudani nzuri wakati wa sherehe za uzinduzi wa Gati

Utamaduni; Wakicheza ngoma ya asili

Vibinti vya Kizenji; Watoto wa kike nao walitoa burudani

Mzee Bakhresa akiwa na Mkuu wa Idara ya Ulinzi ya S.S.B., Abood Mzee Mbwana katika Lounge ya VIP ya Gati hiyo

CREDITS: bIN ZuBEIRY
Download Our App

Post a Comment

CodeNirvana

BLOG RAFIKI

© Copyright EMMANUEL SHILATU - BREAKING NEWS BLOG
Back To Top