Featured
    KWA HABARI NA MATANGAZO EMAIL : pbuyegu2@gmail.com ... Get a superior results by advertising with us by E- Mail us pbuyegu2@gmail.com We will bring Your Business to Light

    Featured Posts

Loading...

WAFUGAJI WANACHANGIA UHARIBIFU WA MAZINGIRA KATAVI

 


DC
Mkuu wa Wilaya ya Mpanda Paza Mwamlima akitoa maagizo kwa wataalamu kuwajibika kila mtu kwa eneo lake ili kuhakikisha anawaletea maendeleo wananchi,Mkuu huyo wa Wilaya alitoa maagizo hayo wakati akifungua kikao cha ushauri Wilaya ya Mpanda kilichofanyika Septemba 30 2013.
(Picha na KIbada Kibada-Mpanda Katavi)
…………………………………………………………………………………..
Na Kibada Kibada –Mpanda Katavi
 Uharibifu wa Mazingira katika wilaya ya Mpanda bado ni changamoto ambayo inaashiria Wilaya ya  Mpanda  uoto wake kuharibika kila kukicha kutokana na uharibifu unaofanyika wa uingizwaji wa mifugo kiholela,ukataji miti,uchomaji moto mapori na uharibifu mwingine wa vyanzo vya maji katika wilaya hiyo.

Hayo yamebainishwa na Mbunge wa Jimbo la Mpanda Vijijini Moshi Selemani Kakoso wakati wa kikao cha ushauri wa wilaya ya Mpanda kilichofanyika kwenye ukumbi wa mikutano wa Halmashauri ya wilaya  ya Mpanda ulioko Idara ya Maji Wilayani  Mpanda.
Mbunge huyo alieleza kuwa  uharibifu wa mazingira na vyanzo vya maji katika maeneo mbalimbali ya Wilaya ya Mpanda unachangiwa na uingizwaji wa mifugo kutoka nje ya wilaya ya Mpanda wanaoingia kinyume na taratibu na kwenda kuvamia maeneo ya vyanzo vya maji.
Alieleza kuwa zaidi ya asilimia 80 ya mifugo kutoka Mikoa ya Mara,Mwanza,Simiyu na Shinyanga imekuwa ikiingia kwa kasi kubwa katika  maeneo ya wilaya ya  Mpanda kupitia mkoa wa Kigoma na Tabora na kuchangia uharibifu mkubwa wa maendeleo.
“Wapo wafugaji wanaoishi kwenye vyanzo vya maji na hao ndio wanaochangia uharibifu wa mazingira katika maeneo mbalimbali Wilayani Mpanda,alitupia lawama Mamlaka husika hususani Idara ya Maliasili kwa kushindwa kuthibiti uharibifu huo wa mazingira kutokana na kuwaacha wafugaji  wanaoishi kwenye vyanzo vyamaji viharibiwe na Mamlaka husika zikiwa zinaangalia bila kuchukua hatua sitahiri.
Akizungumzia Kijiji cha Bugwe ambacho kimetupiwa lawama na kutishiwa kufutwa au  kuhamishwa kwa kile kinachodaiwa kinachangia katika uharibifu wa mazingira alieleza kuwa kijiji hicho wananchi wake hawahusiki  na uharibifu huo bali ni rafiki wa mazingira .
Alieleza kuwa wanao husika na uharibifu huo ni wafugaji na wale wanaojihusisha na shughuli za kilimo na makazi holela  wapo watu ambao wanamakundi makubwa ya ng’ombe walioko katikati ya Tarafa ya Mwese na Kabungu ambapo ni eneo muhimu kwa kuwa ndipo vyanzo vya maji ya mito ipatayo 24,inayotegemewa na wakazi wa Mpanda na Hifadhi ya Taifa ya Wanyama Pori ya Katavi  na mito hiyo ndiyo inayotirirsha maji kuanzia kwenye vyanzo vya maji,ambapo wanyama kama viboko wanahangaika kupata maji na wengine kufa.
Alishauriwa doria ifanyike kwa nguvu kubwa kuwaondoa wavamizi waliovamia katika maeneo vya vyanzo vya maji na kueleza kuwa wengine wanakuja kununua mifugo na kuipeleka katika maeneo ambayo hayaruhusiwi na wapo watu wengi wenye mifugo mingi katika maeneo yanayolalamikiwa ya vyanzo vya maji.
Wapo wajumbe walipendekeza kuwa wapige marufuku kwa mfugaji yeyote,kwa wafugaji kuingiza mifugo katika wilaya ya Mpanda ili kunusuru mazingira na uingizwaji wa mifugo katika wilaya ya Mpanda.
Kwa upande wake Mwanasheria wa Halmashauri ya Wilaya Mpanda Patrick Mwakyusa alikieleza kikao cha Ushauri Wilaya kuwa ni kukiuka katiba ya nchi kumzuia mtu kuishi maeneo yeyote ndani ya jamhuri ya muungano  kwa kuwa nchi ni moja kosa ni kutofuata utaratibu wa matumizi bora ya ardhi.
Akafafanua kuwa sheria ya ardhi ya kijiji imetoa mamlaka ya kupanga matumizi ya ardhi hicho kijiji kinatakiwa kiweke mipango yake ya matumizi bora ya Ardhi ili kuweka maeneo yanayohusika kwa matumizi husika.
Hivyo ili kudhibiti uingizwaji  holela wa mifugo katika vijiji ni kupanga mipango ya matumizi ya ardhi hapo watasaidia kuondoa tatizo la uingizwaji wa mifugo kiholela na kusaidia kuokoa vyanzo vya maji na uharibifu wa mazingira.kwa kutenga maeneo ya matumizi bora ya ardhi katika kijiji husika.
Awali Mkuu wa Wilaya ya Mpanda Paza Mwamlima alieleza alianza kwa kuwasisitiza watumishi wafanye kazi kwa kujituma iwapo watawajibika kila mmoja kwa nafasi yake wataweza kuepusha migogoro inayojitokeza katika utendaji wa kazi kwa kuwa kila mmoja atakuwa anawajibika kwa nafasi yake.
Hivyo aliwasisitiza kila mtu kwa nafasi yae awajibike hapo ndipo matatizo yatapungua au kumalizika kabisa katika maeneo mbalimbali,akizungumzia kuondolewa kwa makazi holela alisema ipo operation inayoendelea kuwaondoa wale wote wanaoishi katika maeno holela yasiyoruhusiwa kwa kuwa kufanya hivyo ni kinyume cha utaratibu wanachangia katika uharibifu wa mazingira.
Download Our App

Post a Comment

CodeNirvana

BLOG RAFIKI

© Copyright EMMANUEL SHILATU - BREAKING NEWS BLOG
Back To Top