Featured
    KWA HABARI NA MATANGAZO EMAIL : pbuyegu2@gmail.com ... Get a superior results by advertising with us by E- Mail us pbuyegu2@gmail.com We will bring Your Business to Light

    Featured Posts

Loading...

MAKAMU WA RAIS DK.. BILAL ATAKA USIMAMIZI WA HAKI ZA BINADAMU UWE JUKUMU LA KILA MTU

 


03 (1)Na Kiza Sungura- MAELEZO
MAKAMU wa Rais Dk. Mohamed Gharib Bilal amesema usimamizi wa haki za binadamu na ujenzi wa maadili mema ndani ya jamii ni jukumu la kila mmoja hivyo kila mmoja ana wajibu wa kulinda kuheshimu na kudumisha haki hizo.
Dk. Bilal ameyasema hayo kwenye Maadhimisho ya Kimataifa ya Haki za Binadamu na Siku ya Kitaifa ya Haki za Binadamu na Maadili katika viwanja vya mnazi mmoja jijini Dar es Salaam jana.
Alismea Watanzania wakishikamana katika hilo, anaamini watashinda kwani umoja ni nguvu katika kuhakikisha kuwa Haki za Binadamu zinalindwa na kupewa nafasi stahiki.
“Nawaasa kujiepusha na mambo yote yanayochangia kwa njia moja ama nyingine kuvunja na kkukiuka misingi ya Haki za Binadamu na Maadili Mema, kuweni raia wema na chukieni maovu” alisema Dk. Bilal.
Makamu wa Rais aliwahakikishia Watanzania kwamba Serikali ya awamu ya nne inatilia maanani sana Haki za Binadamu Utawala Bora na Maadili.

Aliwaasa Watanzania Tanzania kuanzisha kampeni Maalumu za kukuza maadili katika ngazi mbambali zikiwemo za Utumishi wa Umma, Taaisisi za Dini, Elimu na katika maisha ya kila siku.
Alisema suala hilo likifanyika vizuri anaamini Watanzania wote watakuwa wametimiza wajibu wao kwa malezi biora kwa watoto na vijana na kusaidia kupunguza maovu mengi ndani ya jamii.
Alibainisha kuwa Serikali pia imejenga mazingira mazuri na kuruhusu taasisi zisizo za Kiserikali kuanzishwa kwa lengo la kusaidia juhudi zake za kuimarisha Haki za Binadamu hapa nchini.
Alisema hadi kufikia sasa Tanzania ina takribani mashirika 5,000 yasiyo ya Kiserikali na yanayojihusisha na utetezi wa Haki za Binadamu, Mashirika haya yanatambuliwa kwa mujibu wa mikataba mbali mbali ya kimataifa na sharia za nchi.
Naye Naibu Mwanasheria Mkuu wa Serikali George Masaju alisema kuwa  Haki za Binadamu ni kioo cha kuonyesha kuwa nchi yoyote ile imekomaa kidemokrasia, hivyo inaheshimu raia wake kwa kuwapa haki zao za msingi na katioka nchi zenye katiba zilizojengwa katika misingi kidemokrasia kama ya kwetu
Alisema serikali imeamua kuanzisha mpango kazi husika na kuratibu shuhuri hiyo muhimu ya maadhimisho kwa kuhusisha tume mbali mbali za kitaifa.
Download Our App

Post a Comment

CodeNirvana

BLOG RAFIKI

© Copyright EMMANUEL SHILATU - BREAKING NEWS BLOG
Back To Top