Featured
    KWA HABARI NA MATANGAZO EMAIL : pbuyegu2@gmail.com ... Get a superior results by advertising with us by E- Mail us pbuyegu2@gmail.com We will bring Your Business to Light

    Featured Posts

Loading...

MHESHIMIWA ANGELLAH KAIRUKI ATOA MSAADA WA BAISKELI KWA WOTOTO WENYE ULEMAVU WA VIUNGO


1
Mheshimiwa akifafanua jambo kuhusu umuhimu wa kuwajali watoto wenye ulemavu kwa wazazi (hawapo pichani) waliofika kupokea msaada wa baiskeli kwa ajili ya watoto wao. Aidha, katika maelezo yake Mhe. Kairuki aliwasihi wazazi kutowaficha ndani watoto walemavu, bali wawapeleke shule na kuwapatia huduma zingine za muhimu ambaza wao kama binadamu wanatakiwa kuzipata. Pia aliwaomba wadau wengine wajitokeze kuwasaidia watoto wenye ulemavu kwani ni ndugu zetu na wanastajili kusaidiwa. Mheshimiwa Kairuki alitoa jumla ya baiskeli 35 kwa watoto wenye ulemavu wa Kawe, jijini Dar es Salaam
2
Mheshimiwa Kairuki akimkabidhi baiskeli na vifaa mbalimbali mtoto mmojawapo (jina halikufahamika mara moja) ambaye ni mlemavu wa viungo ili imsaidie wakati wa kwenda shuleni na mahali pengine.

3
Mheshimiwa Kairuki akimsikiliza Bi. Blandina Sembu ambaye ni Mratibu wa Shirikisho la Vyama vya Walemavu Tanzania (SHIVYAWATA) alipokuwa akitoa shukrani zake kwa Mhe. Kairuki baada ya kukabidhiwa baiskeli 35 kwa ajili ya watoto wenye ulemavu wa viungo katika Kata ya Kawe.
4
 Mmojawapo wa wazazi wa Kata ya Kawe akimshukuru Mhe. Kairuki (hayupo pichani) kwa niaba ya wazazi wenzake kwa moyo wake wa utoaji na wa kuwajali watoto wenye ulemavu na kuwapatia baiskeli zitakazowasaidia kufika shuleni na mahali pengine kwa urahisi.
5

Baadhi ya watoto wenye ulemavu waliofika kupokea baiskeli hizo kama msaada uliotolewa na Mheshimiwa Kairuki katika harakati zake za kuwasaidia watoto wenye ulemavu.
Download Our App

Post a Comment

CodeNirvana

BLOG RAFIKI

© Copyright EMMANUEL SHILATU - BREAKING NEWS BLOG
Back To Top