Featured
    KWA HABARI NA MATANGAZO EMAIL : pbuyegu2@gmail.com ... Get a superior results by advertising with us by E- Mail us pbuyegu2@gmail.com We will bring Your Business to Light

    Featured Posts

Loading...

SERIKALI YA TANZANIA YAPONGEZWA KWA VITA DHIDI YA RUSHWA.

 



 

D92A3693(1)
Katibu Mkuu Kiongozi Balozi Ombeni Sefue wakiwa katika picha ya Pamoja na Baadhi ya Mabalozi na Wawakilishi wa Mashirika ya Kimataifa nchini Ikulu jijini Dar es Salaam leo jioni(picha na Freddy Maro)

………………………………………………………………………………………

By Freddy Maro

Washirika wa Maendeleo wa Tanzania wakiwemo baadhi ya mabalozi wanaoziwakilisha nchi zao hapa na mashirika ya Kimataifa wameelezea kuridhishwa kwao na juhudi za Serikali ya awamu ya Nne ya Tanzania inaoongozwa na Rais Dkt.Jakaya Kikwete, katika mapambano dhidi ya Rushwa nchini.


 

Hayo yameelezwa na Katibu Mkuu Kiongozi Balozi Ombeni Sefue mara baada ya kukutana na baadhi ya Mabalozi na wawakilishi wa mashirika ya kimataifa ikiwemo Banki ya Afrika,Benki ya Dunia na Shirika la Fedha la Kimataifa(International Monetary Fund) ikulu jijini Dar es Salaam leo jioni.
 

“Yaliyojitokeza katika mkutano huu ni wao kutambua juhudi za serikali yetu kuimarisha vita dhidi ya rushwa ka kuimarisha taasisi zinazohusika moja kwa moja kwa kuziongezea bajeti na kuajiri wafanyakazi wenye uwezo na ujuzi wa kutenda kazi kwa weledi.Ofisi hizi ni pamoja na TAKUKURU yenyewe, ofisi ya mwendesha mashtaka, Mahakama, sekretarieti ya maadili ya umma na polisi,” alisema Balozi Sefue.
 

Katibu Mkuu Kiongozi amesema kuwa washirika hao wa maendeleo wamefurahi kutambua kwamba Serikali imeongeza idadi ya watumishi wa umma wanaofanya kazi katika taasisi zinazohusika na vita vya rushwa nchini na kuboresha utendaji baada ya kupata mafunzo na kwamba miundo mbinu ya taasisi hizi ikwemo majengo ya ofisi na vitendea kazi vimeimarishwa.
 

Balozi  Sefue aliongeza kusema kuwa washirika hao wa maendeleo wamekuwa wawezeshaji wakuu wa taasisi zinazopambana na rushwa nchini kwa kuzichangia kwa fedha na kugharamia mafunzo ya baadhi ya watumishi wa taasisi hizo na kwamba katika mkutano wa leo wameahidi kuendelea kuunga mkono juhudi za Tanzania katika vita dhidi ya Rushwa kwa kuisaidia serikali kuimarisha mifumo, sheria, taratibu na kutoka mafunzo kwa watumishi.
 

Baadhi ya Washirika wa Maendeleo waliohudhuria mkutano wa Katibu Mkuu kiongozi ni pamoja na wawakilishi kutoka Jumuiya ya Ulaya EU, Balozi wa Unigereza nchini, Balozi wa Canada,Balozi wa Norway,Balozi wa Finland, Balozi wa Denmark,Balozi wa Ujerumani, Balozi wa Ireland, Balozi wa Sweden, Mwakilishi wa Ubalozi wa Japan, Mwakilishi wa Benki wa Benki ya Maendeleo ya Afrika, mwakilishi wa Benki ya Dunia na Mwakilishi wa Shirika la Fedha la Kimataifa(IMF).
Download Our App

Post a Comment

CodeNirvana

BLOG RAFIKI

© Copyright EMMANUEL SHILATU - BREAKING NEWS BLOG
Back To Top