Featured
    KWA HABARI NA MATANGAZO EMAIL : pbuyegu2@gmail.com ... Get a superior results by advertising with us by E- Mail us pbuyegu2@gmail.com We will bring Your Business to Light

    Featured Posts

Loading...

WAZIRI CHIKAWE AAHIDI KUBORESHA MASLAHI YA ASKARI POLISI

 



Demetrius Njimbwi – Jeshi la Polisi.

……………………………………………………………………………………

Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi Mhe. Mathias Chikawe ameahidi kuboresha maslahi ya Askari Polisi jambo ambalo litawezesha Jeshi la Polisi kufanya kazi zake kwa ufanisi na hivyo kufanikiwa katika kukabiliana na vitendo vya uhalifu.

New Picture (7)Waziri Chikawe aliyasema hayo jana Makao Makuu ya Polisi wakati alipokuwa akizungumza na maafisa wakuu wa Jeshi hilo kwa lengo la kujitambulisha baada ya kuteuliwa na Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete kuwa waziri wa wizara hiyo. Kikao hicho kilihudhuriwa pia na Naibu Waziri wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya nchi Mhe. Pereila Amme Sillima, Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Mbaraka Abdulwakil, na viongozi mbalimbali wa wizara hiyo.

Aliongeza kuwa, ataishawishi serikali iongeze bajeti ya Jeshi la Polisi ili kuweza kuwajengea askari mazingira mazuri ikiwa ni pamoja na kuboresha maslahi yao. Hii itasaidia kuongeza ufanisi, uaminifu na uadilifu katika utendaji wao wa kila siku jambo ambalo litaleta maendeleo kwa wananchi.


Aidha amewataka wananchi kushirikiana na Jeshi la Polisi katika kutanzua, kubaini na kuzuia vitendo vya uhalifu katika Jamii kabla havijatokea ili kuendelea kudumisha ulinzi na usalama hapa nchini.

Alisema Jeshi la Polisi linahitaji sana ushirikiano kutoka kwa wananchi ambao kwa kiasi kikubwa ndio wanaishi katika jamii ambayo inatendewa uhalifu hivyo kupitia dhana ya polisi jamii na ulinzi shirikishi ni vyema wakaendelea kushirikiana na Jeshi hilo.

Vilevile amelitaka Jeshi la Polisi kuendelea kutoa elimu juu ya sheria za usalama barabarani kwa madereva hususan wa bodaboda ikiwa ni pamoja na kuwachukulia hatua za kisheria wale wote watakaokiuka sheria, kanuni na taratibu hizo.

Kwa upande wake Mkuu wa Jeshi la Polisi Nchini IGP Ernest Mangu, amempongeza Waziri Chikawe kwa kuteuliwa kwake kuwa Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, na kueleza kuwa ana imani kuwa waziri huyo atasaidia katika kuleta mabadiliko ya kiutendaji hasa katika kuongoza mapambano dhidi ya vitendo vya uhalifu pamoja na wahalifu.

IGP Mangu alisema tabia za wananchi kujichulia sheria mkononi ni uvunjifu wa sheria, hivyo wataendelea kuwachukulia hatua za kisheria kwa kuwakamata wote wanaojihusisha na vitendo vya kujichukulia sheria mkononi ili wafikishwe mahakamani.

Katika kikao hicho IGP Mangu, alimkabidhi Waziri Chikawe hati ya mpango wa maboresho unaoelekeza namna ambavyo jeshi la polisi linaendelea kuboreshwa ili kuendana na usasa, weledi na lenye kushirikisha jamii, pamoja na kitabu cha muongozo wa utendaji kazi wa jeshi hilo.
Download Our App

Post a Comment

CodeNirvana

BLOG RAFIKI

© Copyright EMMANUEL SHILATU - BREAKING NEWS BLOG
Back To Top