Featured
    KWA HABARI NA MATANGAZO EMAIL : pbuyegu2@gmail.com ... Get a superior results by advertising with us by E- Mail us pbuyegu2@gmail.com We will bring Your Business to Light

    Featured Posts

Loading...

WIZARA ya Mambo ya Ndani ya Nchi yakusanya bilioni 83.4

 




imagesNa Frank Mvungi- MAELEZO

 WIZARA ya Mambo ya Ndani ya Nchi imefanikiwa kukusanya sh. bilioni 83.4 kufikia mwaka 2013/2014 ambazo zinatokana na shughuli mbalimbali zilizofanywa na Idara ya Uhamiaji.

Hayo yamesemwa na Naibu Waziri wa Wizara hiyo Mh Pereira Ame Silima wakati wa mkutano na waandishi wa habari leo jijini Dar es salaam akieleza mafanikio ya Wizara.

Mh Pereira alibainisha kuwa kwa kipindi cha mwaka 2006/2007 zilikusanywa shilingi bilioni 14.2 ambapo  kumekuwa na ongezeko la bilioni 69.2 kufikia mwaka 2013/2014 ambayo ni moja ya mafanikio ya Serikali ya awamu ya nne.

Mh Pereira alibainisha kuwa Ongezeko hilo ni matokeo ya juhudi zilizofanywa na Serikali katika kuboresha mifumo ya makusanyo ya maduhuli kwenye vyanzo mbalimbali vya Wizara.

Aliongeza kuwa jumla ya magari 192 yalitolewa kwa idara hiyo, 93 yakiwa ni msaada ya wafadhili.

Alitaja vifaa vingine vilivyonunuliwa kwa ajili ya Idara hiyo ni pikipiki 206 na boti mbili (02) ambazo hutumika kufanya misako na doria katika maeneo mbalimbali nchini ikiwa ni hatua za maksudi katika kupambamna na uhalifu.

Kwa upande wa jeshi la Polisi, Mh. Pereira alisema kuwa wamefanikiwa kupunguza uhalifu kutoka makosa 53,268 mwaka 2005 hadi  kufikia 45470 mwaka 2013.

Alitaja sababu kubwa ya kupungua kwa vitendo vya uhalifu nchini kuwa ni ushirikiano mzuri toka kwa wananchi kwa kutumia mfumo wa ulinzi shirikishi,utii wa sheria bila shuruti,vifaa vya kisasa kwa askari yakiwemo magari, pikipiki na boti kwa ajili ya doria.

Wizara ya Mambo ya Ndani ya nchi inaundwa na Jeshi la Polisi,Jeshi la Magereza,Jeshi la Zimamoto na Uokoaji,Idara ya Uhamiaji,Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa,Idara ya Huduma kwa Jamii.
Download Our App

Post a Comment

CodeNirvana

BLOG RAFIKI

© Copyright EMMANUEL SHILATU - BREAKING NEWS BLOG
Back To Top