Featured
    KWA HABARI NA MATANGAZO EMAIL : pbuyegu2@gmail.com ... Get a superior results by advertising with us by E- Mail us pbuyegu2@gmail.com We will bring Your Business to Light

    Featured Posts

Loading...

JUMLA YA WANAWAKE 11 HUFARIKI DUNIA KILA SIKU KWA UGONJWA WA SARATANI YA MLANGO WA UZAZI

 

Mgeni  rasmi  katibu  tawala  wa mkoa wa Iringa Wamoja  Ayub  akifungua mkutano  huo
 
WANAWAKE  11 nchini  hupoteza maisha  kwa ugonjwa wa  saratani  ya mlango wa   kizazi kila  siku  huku wanawake 6000 hugundulika kuwa na ugonjwa  wa  saratani ya mlango wa  kizazi kila mwaka .
 
Mkurugenzi mtendaji  wa T-MARC Tanzania Bi Diana Kisaka  aliyasema hayo leo katika ukumbi  wa VETA  wakati  wa  ufunguzi  mkutano wa  uzinduzi wa mradi wa  kuzuia na  kudhibiti saratani ya mlango wa kizazi mkoani
Iringa.
 
Alisema kuwa jambo la kusikitisha zaidi ni  kuwa takribani wanawake 4000 nchini hupoteza maisha  kila mwaka kutokana na ugonjwa  huo ambapo ni sawa na wastani wa  wanawake hao  11 kwa siku  hupoteza maisha  yao.
 
Hata  hivyo  alisema  kuwa takwimu kutoka Hospital ya  Ocean Road zinaonyesha  kuwa asilimia 40 ya  vifo  hivyo  vinavyotokana na matatizo ya  saratani ni wagonjwa wa saratani ya mlango wa kizazi , huku  takwimu  hizo pia zinaonyesha kuwa asilimia 80 ya  wagonjwa wote wanmaokwenda kwenye matibabu ya  saratani ya malango wa  kizazi fufika  Hospital  kupata  huduma  hiyo kwa kuchelewa  zaidi.
 
Alisema   kuwa kwa ujumla  ugonjwa  wa Saratani ni  tatizo kubwa sana ulimwenguni na hasa katika nchi zinazoendelea ambapo  takwimu  za kimataifa zinaonyesha kuwa kila mwaka zaidi ya watu  milioni 5 hugundulika kuwa na saratani na kufanya tatizo  hilo  kufikia asilimia 29 huku kati yao hupatikana na saratani ya mlango  wa kizazi na kwa bahati mbaya Tanzania ni miongoni mwa nchi zenye tatizo kubwa la ugonjwa  huo.
 
Bi Kisaka  alitaja baadhi ya  sababu  zinazochangia  tatizo hili nchini  ni  pamoja na ukosefu wa taarifa kuhusu umuhimu  wa  watu kuchunguza afya zao mara kwa  mara watu  wengi  husubiri hadi hali  yao ya  afya
iwe mbaya  sana  kabla  ya kutafuta huduma za  uchunguzi na  matibabu Hospitalini .
 
Sababu  nyingine ni  pamoja na imani potofu na kukosa  taarifa  halisi  kuhusu saratani na matibabu ya saratani ,hasa  matibabu ya mionzi ,upungufu wa  huduma za  uchunguzi na  matibabu ya  saratani ,upungufu wa  wataalam
wa  afya pamoja na ufinyu wa bajeti na  upungufu wa fedha za kukidhi mahitaji ya  huduma za kuzuia na kudhibiti saratani ya  mlango wa  kizazi.
Alisema  kwa  kutambua ukubwa wa  tatizo hilo T-MARC  kama asasi  isiyo kuwa  ya  kiserikali ambayo inajishughulisha na uboreshaji  wa afya ya watanzania  kwa kushirikiana na serikali kupitia wizara   ya  Afya na 
ustawi wa jamii  pamoja na wadau mbali mbali wa sekta ya  umma ,sekta binafsi ,wadau wa  kimataifa ,asas za kijamii na watanzania wote kwa ujumla  kwa kuanza  kupambana  na tatizo  hilo.
Na Francis Godwin Blog
Download Our App

Post a Comment

CodeNirvana

BLOG RAFIKI

© Copyright EMMANUEL SHILATU - BREAKING NEWS BLOG
Back To Top