Featured
    KWA HABARI NA MATANGAZO EMAIL : pbuyegu2@gmail.com ... Get a superior results by advertising with us by E- Mail us pbuyegu2@gmail.com We will bring Your Business to Light

    Featured Posts

Loading...

Mama Makinda atoa darasa kwa wanawake kuchangia hoja za nguvu

 


anne-makinda
 
Na Magreth Kinabo –MAELEZO, Dodoma.
Mjumbe wa Bunge Maalum la Katiba, Anne Makinda ametoa changamoto kwa wajumbe wenzake wanawake walio kwenye Bunge hilo, kujenga hoja zenye nguvu zinazohusu masuala yanayohusu wanawake na kuzitetea  kwa sauti moja ili ziweze kupita katika Rasimu ya Katiba.
 
Kauli hiyo imetolewa leo na Mhe. Anne ambaye pia ni Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania  wakati akitoa mchango wake  kwa  wajumbe  wa semina ya kujenga agenda muhimu kwa masuala ya kijinsia iliyoandaliwa na Umoja  wa Wabunge  Wanawake wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania (TWPG) kwa wajumbe wanawake wa Bunge hilo, iliyofanyika kwenye Ukumbi wa Pius Msekwa.
 
“ Ninawaomba  tuwe na hoja zenye nguvu wakati wakuchangia mjdala wa Rasimu ya Katiba . Tukisimama kwa  hoja za nguvu na kutetea vifungu vinavyohusu masuala ya wanawake tunaweza kubadilisha vifungu. Tuzungumzeni hoja tuache kufanya fujo, tusiingie katika malumbano ambayo hayana tija, tuache kuzomea tukifanya hiyo tutakuwa tumejijengea heshima,” alisema Mama Anne.
 
Kwa  upande wake mmoja wa mtoa mada katika semina hiyo,kuhusu haki za wanawake, utu, hali ya maisha na mgawanyo wa rasilimali,  Ussu Mallya, ambaye pia ni wanaharakati wa masuala ya wanawake aliwataka wajumbe hao ,wanawake  kutetea saula la   Usawa wa Kijinsia liingizwe katika Rasimu ya  Katiba likiwa ni moja ya Tunu za Taifa. 
 
Mtoa mada mwingine  ambaye pia mjumbe Bunge hilo na  ni Makamu Mwenyekiti wa TWPG, Suzan Lyimo alisema ni vema wanawake hao kupigania asiliamia 50 inakuwepo ili kuhakikisha masuala yote yanayohusu wakina mama yakuwemo, mfano kwenye nafasi za ubunge, ajira  na ngazi zingine za maamuzi.
Suzan alisema hayo  wakati akitoa mada kuhusu Uwakilishi wa wanawake, katika Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
 
Mada nyingine  iliyotolewa katika semina hiyo ni  masuala ya miradhi na  ndoa iliyotolewa na Victoria  Mandari kutoka Chama cha Wanasheria Wanawake  Tanzania(TAWLA) ambaye aliwataka wajumbe hao kutoendeleza mambo ya mila na desturi ambayo yanamkandamiza mwanamke.
Katika semina hiyo,   baadhi ya wanawake hao walipendekeza masuala ya haki ya  elimu kwa wanawake, haki za uzazi salama, haki ya kumiliki mali, haki ya ulinzi kwa wanawake na watoto, haki ya mtoto wa nje ya ndoa, umri wa mtoto kuolewa kuwa ni miaka 18 kuingia katika rasimu hiyo.
Download Our App

Post a Comment

CodeNirvana

BLOG RAFIKI

© Copyright EMMANUEL SHILATU - BREAKING NEWS BLOG
Back To Top