SPIKA
wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Anne Makinda amesema ni
marufuku kwa Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa) kufanya shughuli zake
ndani ya Bunge la Bajeti.
Alisema
hayo juzi bungeni baada ya Kiongozi wa Kambi ya Upinzani Bungeni
Freeman Mbowe kutangaza baraza kivuli la mawaziri na kusema hicho ndiko
kikosi cha ukawa ndani ya Bunge.
Spika
Makinda alimtaka Mbowe kuhakikisha Ukawa inafanya kazi zake nje ya Bunge
na si ndani ya Bunge kwani wanapokuwa ndani ya Bunge wanakuwa ni kambi
ya upinzani bungeni na si vinginevyo.
Pia Spika Makinda alilitaka baraza hilo kivuli kutoa ushirikiano na wabunge wengine ili kufanya kazi ya kuendeleza watu.
Uteuzi
huo ulihusisha vyama vya Chadema, CUF na NCCR Mageuzi ambapo baraza hilo
kivuli lina mawaziri 29 ambapo watashika nafasi za uongozi katika
kipindi kilichobaki kuelekea uchaguzi mkuu mwakani.
Post a Comment