Featured
    KWA HABARI NA MATANGAZO EMAIL : pbuyegu2@gmail.com ... Get a superior results by advertising with us by E- Mail us pbuyegu2@gmail.com We will bring Your Business to Light

    Featured Posts

Loading...

ITALIA NJE, ENGLAND YAAMBULIA POINTI 1 BRAZIL. .... SUAREZ AFANYA YAKE KAMA KAWA


Mkongwe wa Italia, Andrea Pirlo (kushoto) akibadilishana jezi na Edisnon Cavani wa Uruguay baada ya mechi.
ITALIA imeaga Kombe la Dunia nchini Brazil baada ya kufungwa 1-0 na Uruguay, bao pekee la Diego Godin katika mchezo ambao mshambuliaji Luis Suarez alimng’ata Giorgio Chiellini.
Godin alifunga bao hilo dakika ya 81 na kipa Buffon wa Italia alilazimika kuingia uwanjani dakika ya mwisho kusaidia nguvu ya kusaka bao, Azzuri ikihtaji sare tu kusonga mbele.
Italia ilimpoteza mchezaji wake Marchisio aliyetolewa kwa kadi nyekundu baada ya kumchezea rafu Arevalo Rios dakika ya 60.

Katika mechi nyinine,Costa Rica imemaliza kileleni mwa Kundi D baada ya sare ya 0-0 na England leo ikifikisha pointi saba, Uruguay pointi sita na Italia pointi tatu, wakati England imeondoka na pointi moja.
Kikosi cha Italia kilikuwa; Buffon, Barzagli, Bonucci, Chiellini, Marchisio, De Sciglio, Verratti/Motta dk75, Pirlo, Darmian, Balotelli/Parolo dk46 na Immobile/Cassano dk71.
Uruguay: Muslera, Caceres, Gimenez, Godin, A.Pereira/Stuani dk63, Gonzalez, Arevalo Rios, Rodriguez/Ramirez dk78, Lodeiro/M Pereira dk46, Cavani na Suarez.
Download Our App

Post a Comment

CodeNirvana

BLOG RAFIKI

© Copyright EMMANUEL SHILATU - BREAKING NEWS BLOG
Back To Top