Staa wa sinema za Kibongo, Kajala Masanja amefunguka kuwa yuko Bongo kwa kuwa ndipo nyumbani kwao lakini hana hamu ya kuendelea kuishi nchini kutokana na kuzushiwa mambo kila kukicha.
Akizungumza
na Risasi Mchanganyiko wikiendi iliyopita, mwigizaji huyo alisema
anapenda awe na maisha ya furaha na wanawake wenziye kwa kubadilishana
mawazo ya hapa na pale lakini kwa sasa hana upendo huo kwa kuwa kuna
watu wanaishi kwa kutegemea bifu.
“Unajua
inauma sana, unaenda klabu unamkuta mtu ambaye huko nyuma alikuwa
shoga’ko, kula, kuvaa na kila aina ya ushirikiano mnapeana, sasa mnakuja
kugombana, kiukweli roho huwa inauma ndiyo maana nashindwa hata kwenda
klabu kuepusha mengi, nasubiria viza yangu itoke nisepe zangu China,” alisema Kajala.
Kwa muda mrefu kumekuwa na ugomvi usiokwisha kati ya Kajala na mwigizaji mwenzake, Wema Sepetu.
Kwa muda mrefu kumekuwa na ugomvi usiokwisha kati ya Kajala na mwigizaji mwenzake, Wema Sepetu.
Post a Comment