Baada ya mvua kubwa iliyonyesha Recife na kusababisha mafuriko kutishia
kuahirishwa kwa mechi baina ya Ujerumani na Marekani, hatimaye hali ya
anga ilikuwa murwa kwa mechi hiyo ilikuwa ikisubiriwa kwa hamu haswa kwa
Marekani ambao walikuwa wanahitaji sare ya aina yeyote na kuomba kuwa
Black stars ya Ghana wanakunguwaa iliwao waweze kusonga mbele ktika
kundi G.
Na baada ya mbivu na mbichi kubainika Ujerumani na Marekani zote
zilijikatia tikiti ya kushiriki mechi za raundi ya pili licha ya
Ujerumani kushinda mechi hiyo kwa bao moja bila ya jibu.
Mshambulizi huyo wa Bayern Munich aliifungia Ujerumani bao lake la 9 katika mechi sawa na hizo .
Fauka
ya mvua kubwa iliyonyesha mapema taswira katika uwanja wa Arena
Pernambuco ulioko Recife ilikuwa n ushindani mkubwa baina ya Marekani na
Ujerumani.
Kufuatia
matokeo hayo Marekani sasa watakwenda el Salvador ilikuchuana na
Ubeljiji jumanne ijayo katika mechi yao ya kundi la pili huku Washindi
wa kundi hilo Ujerumani wakiratibiwa kumaliza udhia dhidi ya mshindi wa
pili katika kundi H yaani ( Algeria ama Urusi)
Post a Comment