Malkia
wa Swaziland Mheshimwa Nomsa Matsebula akisalimiana na Mkuu wa Wilaya
ya Rufiji Ndugu Nurdin Babu mara baada ya helikopta iliyomchukua kutua
kwenye uwanja wa Shule ya Sekondari ya Nyamisati huko wilayani Rufiji
ambako alikwenda kutembelea Shule ya Wamanakayama inayomilikiwa na
Taasisi ya Wanawake na Maendeleo,WAMA. Tarehe 2.7.2014. Kulia ni Mke wa
Rais na Mwenyekiti wa WAMA Mama Salma Kikwete.
Mke wa Mfalme Mswati III wa Swaziland Malkia Nomsa Matsebula akisalimiana na Mwenyekiti wa Bodi ya Shule ya Sekondari ya Wamanakayama Dkt. Ramadhan Dau mara baada ya mgeni huyo kuwasili huko Nyamisati tarehe 2.7.2014.
Mke wa Rais na Mwenyekiti wa WAMA Mama Salma Kikwete akimshuhudia Malkia wa Swaziland Nomsa Matsebula akiweka saini kwenye kitabu cha wageni mara baada ya kuwasili Shule ya Sekonadri Wamanakayama.Mwanafunzi Assia Idd akimwonyesha Malkia Matsebula kutoka Swaziland namna ya kutumia i-pad kwenye masomo ya sayansi na hesabu wakati Malkia huyo alipotembele Shule ya Sekondari ya Wamanakayama inayomilikiwa na Taasisi ya WAMA inayoongozwa na Mke wa Rais Mama Salma Kikwete.Malkia wa Swaziland Nomsa Matsebula akipanda mti wa kumbukumbu ya kutembelea Shule ya Sekondari ya Wasichana Wamanakayama iliyoko katika Kijiji cha Nyamisati katika wilaya ya Rufiji.Mke wa Mama Salma Kikwete akimpokea Mgeni wake Malkia wa Swaziland Nomsa Matsebula mbele ya jengo la ofisi ya Taasisi ya Wanawake na Maendeleo,WAMA.Mama Salma Kikwete akimkabidhi mgeni wake zawadi ya picha.
Mke wa Mfalme Mswati III wa Swaziland Malkia Nomsa Matsebula akisalimiana na Mwenyekiti wa Bodi ya Shule ya Sekondari ya Wamanakayama Dkt. Ramadhan Dau mara baada ya mgeni huyo kuwasili huko Nyamisati tarehe 2.7.2014.
Malkia
wa Swaziland Nomsa Matsebula akiwa amefuatana na mwenyeji wa Mama Salma
Kikwete akiwapungia wananchi wa Kijiji cha Nyamisati waliofika kumlaki
mara baada ya helikopta iliyomleta kutua kwenye uwanja wa Shule ya
Sekondari ya Nyamisati tarehe 2.7.2014.
Mke wa Rais na Mwenyekiti wa WAMA Mama Salma Kikwete akimshuhudia Malkia wa Swaziland Nomsa Matsebula akiweka saini kwenye kitabu cha wageni mara baada ya kuwasili Shule ya Sekonadri Wamanakayama.Mwanafunzi Assia Idd akimwonyesha Malkia Matsebula kutoka Swaziland namna ya kutumia i-pad kwenye masomo ya sayansi na hesabu wakati Malkia huyo alipotembele Shule ya Sekondari ya Wamanakayama inayomilikiwa na Taasisi ya WAMA inayoongozwa na Mke wa Rais Mama Salma Kikwete.Malkia wa Swaziland Nomsa Matsebula akipanda mti wa kumbukumbu ya kutembelea Shule ya Sekondari ya Wasichana Wamanakayama iliyoko katika Kijiji cha Nyamisati katika wilaya ya Rufiji.Mke wa Mama Salma Kikwete akimpokea Mgeni wake Malkia wa Swaziland Nomsa Matsebula mbele ya jengo la ofisi ya Taasisi ya Wanawake na Maendeleo,WAMA.Mama Salma Kikwete akimkabidhi mgeni wake zawadi ya picha.
PICHA NA JOHN LUKUWI
wanafunzi
Elizabeth Kipoto anayesoma kidato cha tatu katika Shule ya Sekondari ya
wasichana ya Wamanakayama akiwaonyesha wageni jaribio la kujua kama
kuna protini kwenye vyakula katika maabala ya Biologia shuleni hapo
*********
Mke wa Mfalme wa Swaziland Malkia
Nomsa Matsebula ameipatia shule ya Sekondari ya WAMA- Nakayama iliyopo
kijiji cha Nyamisati wilaya ya Rufiji mkoani Pwani zaidi ya shilingi
milioni tano ili ziweze kuwasaidia wanafunzi wa shule hiyo katika
mahitaji yao ya kila siku. Malkia Matsebula ambaye ni Mke wa Mfalme Muswati alitoa fedha hizo jana wakati alipoitembelea shule hiyo ambayo ni ya bweni inayopokea Watoto yatima na wanaotoka kwenye familia maskini kutoka mikoa yote ya Tanzania Bara na Visiwani.
Akiongea na wanafunzi hao Malkia Matsebula aliwataka wanafunzi hao kutumia nafasi hiyo kusoma kwa bidii kwani msichana ni mtu anayeyashika maisha yake ya baadaye katika mikono yake kwa kujenga nyumba ya upendo, kufanya kazi zake vizuri kwa kuona jamii yake inakuwa.
Aliwataka kusoma masomo ya aina mbalimbali ili hapo baadaye waweze kuwa na taaluma mbalimbali zikiwemo za ujenzi, injinia ,sheria, uhasibu kwani elimu haitoki katika mti bali ni mpangilio ambao mwanafunzi anajipangia.
“Kumbukeni kuwa Elimu haipatikani shuleni peke yake bali hata katika jamii inayowazunguka kwani kwenda shule siyo kama umeelimika bali unatakiwa kuvifanyia kazi vile ambavyo umejifunza, wanawake onyesheni elimu yenu kwa vitendo ili jamii inufaike na elimu hiyo.
Wanawake ni watu wanaopenda jamii ingawa wanakutana na matatizo mbalimbali ikiwa ni pamoja na ndoa za utotoni, kuacha shule, unyanyasaji wa kijinsia kwani bila ya wao hakuna maendeleo katika nchi , nyinyi tumieni nafasi hii kusoma kwa bidii ili hapo baadaye muweze kuzitatua changamoto hizo”, Malkia Matsebula alisema.
Aliwasihi wanafunzi hao kujenga tabia ya kujiheshimu katika maisha yao ikiwa ni pamoja na jinsi ya kuongea na kuvaa mavazi ya heshima na kuheshimu wengine kwani Elimu inakuja kwa kujiheshimu.
Aidha Malkia Matsebula aliwaomba wadau wengine wa maendeleo kumuunga mkono Mke wa Rais Mama Salma Kikwete kuwasaidia watoto hao ili waweze kupata elimu jambo ambalo litasaidia kupatikana kwa viongozi na wanawake wengi wasomi hapo baadaye.
Kwa
upande wa walimu aliwataka kuwafundisha wanafunzi hao Historia ya nchi
yao na Bara la Afrika kwa ujumla ili wajue ni wapi walikotoa na viongozi
wao walikuwa wanafanya mambo gani. Kwa kufanya hivyo wataweza kuilinda
na kuitetea nchi na bara lao.
Naye Mke
wa Rais Mama Salma Kikwete alimshukuru Malkia Matsebula kwa kutembelea
shule hiyo na kusema kuwa tafiti zinaonyesha kuwa kama mtoto wa kike
atapata elimu ya kutosha tatizo la ndoa za utotoni, vifo vitokanavyo na
uzazi na vifo vya watoto wenye umri wa chini ya miaka mitano
vitapungua.
Mama
Kikwete ambaye pia ni Mwenyekiti wa Taasisi ya Wanawake na Maendeleo
(WAMA) ambayo ndiyo inayoendesha shule hiyo; alisema walichagua elimu
kwa mtoto wa kike kuwa moja ya kazi zinazofanywa na yake kwa
kuamini kuwa elimu ni ufunguo wa maisha ambayo mwanamke alikuwa
ameikosa kwa muda mrefu.
“Taasisi
ya WAMA iliamua kujenga shule hii ili kuweza kutoa elimu kwa watoto wa
kike ambayo ni yatima na wanatoka katika mazingira hatarishi kwani
watoto hawa walikosa nafasi ya kusoma ukilinganisha na watoto wengine”,
alisema Mama Kikwete.
Shule
hiyo ya kidato cha kwanza hadi cha nne ilianza mwaka 2010 ikiwa na
wanafunzi 83 hadi sasa idadi ya wanafunzi imekuwa na kufikia 336 na
katikati ya mwezi huu inampango wa kuanzisha kidato cha tano na cha
sita.
Licha ya
kutembelea shule ya Sekondari ya WAMA-Nakayama Malkia Matsebula
aliitembelea Taasisi ya WAMA iliyopo wilaya ya Ilala jijini Dar es
Salaam na kujionea kazi mbalimbali zinazofanywa na Taasisi hiyo pia
alishiriki chakula cha jioni kilichoandaliwa na mwenyeji wake Mama Salma
Kikwete.
Post a Comment