Na Shija Felician
Kahama
JESHI la Polisi wilayani
Kahama mkoani Shinyanga linamshikiria Mwenyekiti wa Umoja wa Vijana wa CCM
[UVCCM]mkoani Shinyanga Mapinduzi Mabula kwa tuhuma ya kufanya fujo na kuharibu
mali.
Kwa mujibu wa taarifa za
Polisi zilizothibitishwa na Kaimu Kamanda wa Polisi mkoa wa Shinyanga,Kihenya
Kihenya,Mabul;a ambaye pia ni Mfanyakazi wa Mamlaka ya Mapato Tanzania mkoani
Shinyanga TRA amekamwatwa jana jioni.
Katika tukio hilo
Mapinduzi alifika mjini Kahama akitokea Shinyanga na kisha kukodi taxi namba T
992 CGQ iliyokuwa ikiendeshwa na Nicholaus Bilambona ambapo alikataa kulipa
hali iliyozua vuruga iliyopelekea Kiongozi huyo wa UVCCM kuvunja vioo vya gari
hiyo.
Hata hivyo Mabula alikamatwa
na Polisi na kufikishwa kituoni ambapo napo alifanya fujo akigoma kuingizwa
mahabusu mpaka pale askari walipotumia nguvu ya ziada kumweka chini ya Ulinzi
kwenye chumba cha kuhifadhia wahalifu.
Wakati leo mchana kipindi
hiki kikitoka Kituo cha Polisi Kahama Mtuhumiwa alikuwa bado mahabusu huku jitihada
za kumtoa kwa dhamana zilizokuwa zikifanywa na UVCCM wilaya ya Kahama
zikiendelea ingawa kesho asubuhi anatarajiwa kufikishwa mahakamani kujibu tuhuma
zake .
Post a Comment