Featured
    KWA HABARI NA MATANGAZO EMAIL : pbuyegu2@gmail.com ... Get a superior results by advertising with us by E- Mail us pbuyegu2@gmail.com We will bring Your Business to Light

    Featured Posts

Loading...

VAN GAAL AMCHINJILIA MBALI MBELGIJI MAROUANE FELLAINI, ASEMA SIO AINA YA MCHEZAJI WA MAN UNITED

 

Audition: United hope Marouane Fellaini's displays in Brazil will help them recoup their £27m investment

KOCHA wa Manchester United, Louis Van Gaal amemuagiza mkurugenzi mkuu wa klabu hiyo, Ed Woodward, kumuuza  Marouane Fellaini kwa madai kuwa sio aina ya mchezaji anayetakiwa kukipiga Old Trafford.
Fellaini ameonesha kiwango kizuri katika fainali za kombe la dunia na kuibua maswali kama Van Gaal ataendelea kumbakisha nyota huyo aliyesajiliwa na David Moyes kwa ada ya uhamisho ya paundi milioni 27 kutoka Everton.
Lakini tayari Van Gaal ameshaagiza kuuzwa kwa mchezaji huyo kabla msimu mpya haujaanza.
MPENJA BLOG inafahamu Van Gaal amewaambia watu wanaohusika na Fellaini kuwa 'sio aina ya mchezaji wa Man United".
Vyanzo vya habari kutoka Old Trafford wiki hii vimeeleza kuwa Van Gaal ameweka wazi nani anamtaka na nani hamtaki katika kikosi chake na tayari amemwambia Ed Woodward.
Lakini inaonekana United haitaweza kumuuza Fellaini kwa kiwango cha paundi milioni 27 kama wao walivyomnunua kutoka Everton mwezi septemba mwaka jana.
Boost: Belgium's Marouane Fellaini has enjoyed something of a renaissance at World Cup
Ameimarika: Mchezaji wa Ubelgiji,  Marouane Fellaini angalau amefurahia kombe la dunia nchini Brazil.

Kocha aliyetimuliwa Man United, David Moyes alimlinda Fellaini msimu ulipoita na alikuwa anasema nyota huyo mwenye miaka 26 alikuwa na kiwango kizuri, lakini hakuizoea  United.
Kwasasa kama Fellaini anataka kuichezea United msimu ujao anatakiwa kuonesha kiwango cha juu katika mechi zilizosalia za kombe la dunia.
Ruthless: Louis van Gaal has made it clear which players he wants when he takes charge at United
Hana huruma akiwa kazini: Louis van Gaal ameweka wazi wachezaji wanaowataka mara atakapoanza kazi.
Download Our App

Post a Comment

CodeNirvana

BLOG RAFIKI

© Copyright EMMANUEL SHILATU - BREAKING NEWS BLOG
Back To Top