KOCHA
wa Manchester United, Louis Van Gaal amemuagiza mkurugenzi mkuu wa
klabu hiyo, Ed Woodward, kumuuza Marouane Fellaini kwa madai kuwa sio
aina ya mchezaji anayetakiwa kukipiga Old Trafford.
Fellaini
ameonesha kiwango kizuri katika fainali za kombe la dunia na kuibua
maswali kama Van Gaal ataendelea kumbakisha nyota huyo aliyesajiliwa na
David Moyes kwa ada ya uhamisho ya paundi milioni 27 kutoka Everton.
MPENJA BLOG inafahamu Van Gaal amewaambia watu wanaohusika na Fellaini kuwa 'sio aina ya mchezaji wa Man United".
Vyanzo
vya habari kutoka Old Trafford wiki hii vimeeleza kuwa Van Gaal ameweka
wazi nani anamtaka na nani hamtaki katika kikosi chake na tayari
amemwambia Ed Woodward.
Lakini
inaonekana United haitaweza kumuuza Fellaini kwa kiwango cha paundi
milioni 27 kama wao walivyomnunua kutoka Everton mwezi septemba mwaka
jana.
Ameimarika: Mchezaji wa Ubelgiji, Marouane Fellaini angalau amefurahia kombe la dunia nchini Brazil.
Kocha
aliyetimuliwa Man United, David Moyes alimlinda Fellaini msimu ulipoita
na alikuwa anasema nyota huyo mwenye miaka 26 alikuwa na kiwango
kizuri, lakini hakuizoea United.
Kwasasa
kama Fellaini anataka kuichezea United msimu ujao anatakiwa kuonesha
kiwango cha juu katika mechi zilizosalia za kombe la dunia.
Hana huruma akiwa kazini: Louis van Gaal ameweka wazi wachezaji wanaowataka mara atakapoanza kazi.
Post a Comment