Featured
    KWA HABARI NA MATANGAZO EMAIL : pbuyegu2@gmail.com ... Get a superior results by advertising with us by E- Mail us pbuyegu2@gmail.com We will bring Your Business to Light

    Featured Posts

Loading...

WANANCHI KATA YA MWENDAKULIMA WANYWA MAJI YALIYOCHANGANYIKA NA KINYESI CHA BINADAMU.


PICHA KUTOKA MAKTABA
Na Shija Felician
Kijukuu Blog Kahama

Maisha ya wananchi wa kata ya mwendakulima wanaozunguka mgodi wa Buzwagi wilayani Kahama mkoani Shinyanga yako hatarini kukumbwa na magonjwa ya mlipuko kutokana na kunywa maji yenye mchanganyiko na kinyesi cha binadamu  
 
Hali hiyo imebainishwa leo kwenye mkutano wa hadhara wa kamati ya bunge Ardhi maliasili na mazingira ambao wananchi hao walihoji uhalali wa walinzi wa mgodi wa Buzwagi kumwaga maji safi yanayochotwa kwenye eneo linalomilikiwa na mgodi huo
 
Katika mkutano huo wananchi hao wamedai maeneo ya visima vya kuchota maji yamebanwa na matumizi ya kibinadamu hali ambayo baadhi ya vinyesi vya binadamu hutiririka na kujichanganya kwenye maji hayo hali ambayo ni hatari kwa maisha ya binadamu
 
Walisema kutokana na hali hiyo visima vyenye maji safi na salama viko kwenye eneo linalomilikiwa na mgodi wa Buzwagi lakini wananchi wakienda kuchota humo maji hayo humwagwa na walinzi wa mgodi huo
 
Hata hivyo malalamiko hayo mwenyekiti wa kamati hiyo James Lembeli amemtaka naibu waziri wa bunge Ardhi maliasili na mazingira Ummy Mwalimu kulitolea ufafanuzi lalamiko hilo kwa kuwa suala la uchafuzi wa maji liko kwenye wizara yake
 
Kwa upande wake naibu waziri huyo aliyekuwa ameambatana na kamati hiyo kuzungukia migodi ya dhahabu amesema suala la ujenzi wa visima vya maji salama sio la mgodi bali ni la halimashauri yao ya mji ni suala la serikali ya kijiji kupeleka mipango kazi ya kujengewa visima
Download Our App

Post a Comment

CodeNirvana

BLOG RAFIKI

© Copyright EMMANUEL SHILATU - BREAKING NEWS BLOG
Back To Top