Featured
    KWA HABARI NA MATANGAZO EMAIL : pbuyegu2@gmail.com ... Get a superior results by advertising with us by E- Mail us pbuyegu2@gmail.com We will bring Your Business to Light

    Featured Posts

Loading...

Lowassa, Mbowe Watoa Mkono Wa Pole Kwa Waathirika wa Mafuriko Shinyanga


Waziri Mkuu mstaafu, Edward Lowassa na mwenyekiti wa  Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Freeman Mbowe, wametoa salamu za pole na rambirambi kwa wananchi wa kijiji cha Mwakata wilayani Kahama walioathirika na mvua ya mawe na upepo mkali hivi karibuni.

Akizungumza kwa niaba ya Lowassa ambaye pia ni mbunge wa Monduli, mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) mkoa wa Shinyanga, Hamis Mgeja, alisema mbunge huyo ametoa rambIrambi ya Sh. milioni tano kwa ajili ya wananchi wote walioathirika.

“Naungana na wananchi wote kwa kuwapa salamU za pole na rambirambi baada ya kutokea janga hilokubwa lilipoteza watu wengi na mali…tupo pamoja katika kipindi hiki cha majonzi,” alisema Mgeja kwa niaba ya Lowassa.

Alisema atazidi kushirikiana na wananchi hao katika maombi ili wale waliojeruhiwa katika tukio hilo waweze kurejea katika hali yao ya kawaida.

Lowassa alisema Tanzania ni moja, wananchi wake ni wamoja hivyo lazima katika kipindi hiki wawe wamoja na kuepukana na minong’ono yoyote inayoweza kuwatenganisha katika umoja wao.

Mgeja alisema pamoja na kuwapo na maneno maneno awali kati ya viongozi wa serikali na chama, lakini chama chake hakina matatizo yoyote kwa sasa kutokana na serikali kuanza kutimiza majukumu yake.

“Chama hakina matatizo na serikali ya mkoa ama wilaya, lakini ilikuwa ni kukumbushana kuwatumikia wananchi hawa kipindi walichopatwa na janga lile…tushirikiane ili kurejesha hali nzuri kwa watu hawa,” alisema Mgeja. 
 
Naye mwenyekiti wa Chadema, Mbowe, alisema chama chake kinaungana na Watanzania wote katika kuomboleza janga hilo lililoathiri watu wengi katika kijiji cha Mwakata.

“Tusiingize siasa katika jambo hili bali tunachotakiwa tuungane wote huku serikali ikiwa na jukumu la kuhakikisha ina wajibu  wa kuwahudumia watu hawa,” alisema Mbowe.

Mbowe alisema chama chake kinatoa rambirambi ya Sh.milioni 10 kwa ajili ya waathirika hao, lakini alimuomba mkuu wa mkoa wa Shinyanga, Allynassoro Rufunga, pesa hizo aseme wanunue mahitaji gani.

“Kiasi hiki hatuwezi kutoa taslim, bali tunaomba tuelezwe tununue mahitaji yapi ili yawanufaishe wananchi hawa walioathirika na mvua ya mawe na upepo mkali,” alisema. 
 
Aidha, Mbowe alimpa pole mbunge wa jimbo la Msalala, Ezekiel Maige, kutokana na janga hilo kutokana na kutokea ndani ya jimbo lake.

Mkuu wa wilaya ya Kahama, Mpesya, alimshukuru Mbowe kwa niaba ya chama chake kwa kuonyesha ubinadamu kuweza kuwasaidia waathirika hao.

“Hapa hakuna siasa, bali janga hili ni la kila mmoja…Chadema wameonyesha mfano na kuona hakuna itikadi katika majanga, tushirikiane kwa pamoja mheshimiwa Mbowe,” alisema Mpesya.

Naye mkuu wa mkoa wa Shinyanga, Ally Rufunga, aliwashukuru wote waliochangia waathirika hao akiwamo Lowassa na Chadema, huku akimuomba mwenyekiti Mbowe pesa walizotoa wanunulie mabati pamoja na maturubai.
Download Our App

Post a Comment

CodeNirvana

BLOG RAFIKI

© Copyright EMMANUEL SHILATU - BREAKING NEWS BLOG
Back To Top