Featured
    KWA HABARI NA MATANGAZO EMAIL : pbuyegu2@gmail.com ... Get a superior results by advertising with us by E- Mail us pbuyegu2@gmail.com We will bring Your Business to Light

    Featured Posts

Loading...

Mawaziri 11 waanguka CCM



SASA ni dhahiri kuwa mawaziri 11 wa Serikali ya Awamu ya Nne inayomaliza muda wake, wametoswa katika mbio za kuwania ubunge kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), kati yao wakiwemo watatu ambao kura katika majimbo yao zilirudiwa baada ya kulalamikiwa.
Awali katika kura za maoni za kupata wagombea ubunge wa CCM zilizofanyika nchi nzima Agosti mosi mwaka huu, mawaziri tisa waliangushwa katika kinyang’anyiro hicho, akiwemo Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mathias Chikawe (Nachingwea) na Waziri wa Kazi na Ajira, Gaundentia Kabaka (Tarime Mjini).
Mbali na hao, pia walikuwepo naibu mawaziri saba, akiwemo wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mahadhi Juma Maalim, Pereira Ame Silima (Mambo ya Ndani), Amos Makala (Maji), Kaika Saning’o ole Telele (Maendeleo ya Mifugo na Uvuvi), Dk Makongoro Mahanga (Kazi na Ajira), Adam Malima (Fedha) na Pindi Chana (Waziri Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto).
Baada ya kura hizo za maoni, Halmashauri Kuu ya Taifa (NEC) ya CCM iliyokaa wiki hii, ilibaini kuwepo kwa kasoro katika kura za maoni zilizofanyika katika majimbo 11 ambako zililalamikiwa, yakiwemo matatu ya Busega mkoani Shinyanga, Rufiji mkoani Pwani na Mahenge mkoani Iringa ambayo yalikuwa yakiwaniwa na mawaziri watatu.(VICTOR)
Download Our App

Post a Comment

CodeNirvana

BLOG RAFIKI

© Copyright EMMANUEL SHILATU - BREAKING NEWS BLOG
Back To Top