Madai mazito! Kigogo wa Chama cha
ACT-Wazalendo katika Kijiji cha Vitonga Kata ya Malali Wilaya ya Mvomero
mkoani hapa, Coster Peter Makalius (55), anadaiwa kuuawa kikatili na
mgoni wake, Mabula John, chanzo kikielezwa kuwa ni wivu wa kimapenzi.
Tukio hilo la kuhuzunisha lilijiri hivi
karibuni katika Kijiji cha Vitonga eneo la Kidai katikati ya mashamba
yanayomilikiwa na Profesa wa Chuo Kikuu cha Mzumbe aliyetajwa kwa jina
moja la Bujiku ambapo kigogo huyo wa ACT ndiye aliyekuwa msimamizi mkuu
wa mashamba hayo.
Mwanahabari wetu alipofika eneo la tukio
alishuhudia mwili wa Makalius ukiwa umelazwa kwenye majani ya migomba
huku kichwa chake kikiwa kinavuja damu na ubongo baada ya kupigwa na
jembe kichwani huku Mabula naye akiwa hoi kwa kipigo cha raia wenye
hasira kali.
Wakihojiwa na mwandishi wetu mashuhuda
wa tukio hilo, Yohana Ngana na Mogella Kibwana Mihambo walisema: “Sisi
ni miongoni mwa watu tuliokodi mashamba ya Profesa Bujiku.
“Ametukodishia na tunamlipa heka moja
ndoto moja (ndoto ni gunia moja la kilo 100, iwe mpunga au mahindi
inategemea umelima nini) na mashamba hayo msimamizi mkuu alikuwa ni
Makalius.
“Mabula alitakiwa kutoa ndoto lakini cha kushangaza aliinua jembe na kumlima kichwani Makalius.
Kwa upande wake Mwenyekiti wa Kijiji cha Vitonga, Francis Anthony Kinolo alithibitisha kutokea kwa mauaji hayo kijijini kwake.
“Mabula alitakiwa kutoa ndoto lakini cha kushangaza aliinua jembe na kumlima kichwani Makalius.
Kwa upande wake Mwenyekiti wa Kijiji cha Vitonga, Francis Anthony Kinolo alithibitisha kutokea kwa mauaji hayo kijijini kwake.
Baada ya kutoka ofisi ya kata, mwandishi
wetu alifka nyumbani kwa marehemu na kufanikiwa kuzungumza na mtoto wa
marehemu, Evarist Makalius ambapo ndiye aliyebumburua kisa cha mkasa huo
wa kusikitisha kwamba baba yake alikuwa akimtuhumu Mabula kutembea na
mkewe.
“Chanzo cha kifo cha baba ni mama wa kambo ambaye alikuwa na uhusiano wa kimapenzi na Mabula kwa siku nyingi.
“Chanzo cha kifo cha baba ni mama wa kambo ambaye alikuwa na uhusiano wa kimapenzi na Mabula kwa siku nyingi.
Katika ugomvi wao baba anayedaiwa kutembea na mama alidaiwa kumuua baba. Ile ishu ya mashamba ni bosheni tu.
“Chanzo kikuu ni hiki cha wivu wa mapenzi,” alisema Evarist huku akiangua kilio.
Mke huyo wa marehemu, Anna Gasper alipotakiwa kuzungumzia tukio hilo alisema:
“Chanzo kikuu ni hiki cha wivu wa mapenzi,” alisema Evarist huku akiangua kilio.
Mke huyo wa marehemu, Anna Gasper alipotakiwa kuzungumzia tukio hilo alisema:
“Mume wangu alisema anajisikia vibaya,
akanituma niende shamba nikachume nyanya, niliporudi nyumbani naye
akaniaga anakwenda shamba cha ajabu baada ya muda, nilipokea taarifa
kwamba Mabula amemuua mume wangu,” alisema mama huyo.
Alipoulizwa kama alikuwa na uhusiano wa kimapenzi na Mabula alisema anashangaa kusikia watu wakidai hivyo.
Jeshi la polisi mkoani hapa limethibitisha kutokea kwa tukio hilo na kwamba mtuhumiwa atafikishwa mahakamani wakati wowote.
Jeshi la polisi mkoani hapa limethibitisha kutokea kwa tukio hilo na kwamba mtuhumiwa atafikishwa mahakamani wakati wowote.
GPL
Post a Comment