Featured
    KWA HABARI NA MATANGAZO EMAIL : pbuyegu2@gmail.com ... Get a superior results by advertising with us by E- Mail us pbuyegu2@gmail.com We will bring Your Business to Light

    Featured Posts

Loading...

Mkuu wa mkoa apiga marufuku ya mikutano ya kisiasa

Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Chiku Galawa amepiga marufuku mikutano yote ya kisiasa na maandamano ya kisiasa kipindi ambacho Bunge la 11 litaanza.

Katika taarifa yake iliyotolewa kwa vyombo vya habari, amesema kuna maandalizi yanaendelea kuelekea kuanza kwa Bunge la 11 wiki ijayo hamna mikutano ya kisiasa inayoruhusiwa ili kuwe na amani kipindi cha Bunge.

Amesema kuwa amri hiyo pia imetolewa na vyombo vya ulinzi na usalama ili kuthibiti wale wote wenye malengo ya kuharibu amani na utulivu uliopo.

Wabunge wateule wameanza kuwasili Dodoma kwa ajili ya kuapishwa na kusubiria hotuba ya Rais Magufuli pamoja na Uchaguzi wa Spika na Naibu wake.

Galawa amesema yeyote atakaye jaribu kuharibu amani na utulivu uliopo atachukuliwa hatua kali za kisheria.
Download Our App

Post a Comment

CodeNirvana

BLOG RAFIKI

© Copyright EMMANUEL SHILATU - BREAKING NEWS BLOG
Back To Top