Featured
    KWA HABARI NA MATANGAZO EMAIL : pbuyegu2@gmail.com ... Get a superior results by advertising with us by E- Mail us pbuyegu2@gmail.com We will bring Your Business to Light

    Featured Posts

Loading...

NGUVU KUBWA YA POLISI YATUMIKA KUDHIBITI WANAFUNZI

Jeshi la Polisi mkoani Kagera limelazimika kutumia nguvu kuwatawanya wanafunzi zaidi ya mia nane wa kidato cha tano na cha sita katika shule ya sekondari ya Ihungo waliofanya maandamamo yasiyo rasmi wakati wakielekea kwa mkurugenzi mtendaji wa manispaa ya Bukoba kwa lengo la kuelezea matatizo mbalimbali wanayokumbana nayo shuleni hapo yanayohusina na masuala ya chakula, afya na taaluma. 

Jeshi la Polisi lililazimika kutumia nguvu za kuwatawanya wanafunzi hao waliokuwa wakiiba nyimbo mbalimbali huku wapiga kelele baada ya kukaidi maekezo yaliyokuwa yanatolewa na maofisa wa jeshi hilo yaliyokuwa yanawataka watawanyike ili matatizo yao yatafutiwe ufumbuzi.
Awali, wakizungumza wakati wakielezea matatizo yaliyowapekelekea hadi wakafikia uamzi wa kuchukua hatua ya kuandamana kwa lengo la kuonana na mkurugenzi mtendaji wa manispaa ya Bukoba wanafunzi hao wameelezea kuwa wanapewa chakula kisichofaa kwa matumizi ya binadamu na wakati mwingine wanapewa mulo mmoja au milo miwili badala ya milo mitatu iliyopangwa pia wamelalamikia hali ya vyoo kwa kusema vinahatarisha afya zao kwa kuwa ni vibovu na hivyo vinaweza kusababisha mlipuko wa magonjwa.
Naye, Philip Boneventula mkuu wa shule ya sekondari ya Ihungo akizungumza amesema malalamiko ya wanafunzi ni ya kweli, amesema tatizo la chakula linaloikabili shule hiyo linatokana na hatua ya wazabuni ya kusitisha huduma ya usambazaji wa chakula kufuatia deni kubwa wanalodai shule la zaidi ya shilingi milioni mia moja kumi na tatu, huku afisa taaluma wa sekondari katika manispaa ya Bukoba, Wandela Lwakatare kwa niaba ya mkurugenzi mtendaji wa manispaa ya Bukoba akielezea mambo yanayochangia matatizo yanayozikumba shule za sekondari za bweni za serikali ambayo ameyataja kuwa ni pamoja na ucheleweshwaji wa ruzuku.
Download Our App

Post a Comment

CodeNirvana

BLOG RAFIKI

© Copyright EMMANUEL SHILATU - BREAKING NEWS BLOG
Back To Top