Featured
    KWA HABARI NA MATANGAZO EMAIL : pbuyegu2@gmail.com ... Get a superior results by advertising with us by E- Mail us pbuyegu2@gmail.com We will bring Your Business to Light

    Featured Posts

Loading...

HABARI MPYAAAAA ZA JIDE NA DOGODOGO WALIONASWA NAYE ZAVUJA



Legendary wa Bongo Fleva, Judith Wambura Mbibo ‘Jide’ akishow love na Meddy Ahmed ‘Mtoto wa Vitoto’.

LIGI KUU ENGLAND CHELSEA WAZIDI KUTISHA


BINTI ABAKWA HADI KUFA BAADA YA KUDAI PINDA HAWEZI KUWA RAIS TANZANIA


Kati ya mambo makubwa leo katika mitandao ya kijamii hasa Facebook na Twitter ni taarifa ambazo mimi pia nimezipokea kwa mshangao na masikitiko makubwa, ni taarifa kuhusu mauaji ya mwanadada Bettie Ndejembi ambaye amefariki baada ya kubakwa hadi kupoteza fahamu.

AJALI MBAYA YATOKEA TENA MBEYA ..... KUMI WAFARIKI DUNIA NA SABA KUJERUHIWA KATIKA AJALI YA KIPANYA ILIYOTOKEA MBALIZI, MBEYA

 

Hivi ndivyo ambavyo Daladala hiyo ilivyojibamiza muda mchache uliopita 

MTEMVU: CCM ITAUPUKUTISHA UPINZANI TEMEKE UCHAGUZI WA MITAA, SIYO KWA NGUVU ILA KWA MATUNDA YA UTEKELEZAJI ILANI


Mbunge wa Temeke, Abbas  Mtemvu akihutubia mkutano wa hadhara uliofabyika kwenye Uwanja wa shule ya Sokoine, Temeke jijini Dar es Salaam, jana, Agosti 30, 2014.
Mtemvu akishangiliwa wakati akihutubia mkutano huo wa hadhara

NI WAKATI WA JAPAN KUHAMIA AFRIKA – WAZIRI MKUU



PG4A3943Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akizungumza na Naibu Waziri wa Mambo ya Nje wa Japan, Hirotaka Ishihara baada ya kukutana naye Ofisini kwake jijini Dar es salaam August 30, 2014. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
WAZIRI MKUU Mizengo Pinda amesema umefika wakati wa Japan kuhamia barani Afrika na na kuwekeza kwa nguvu hasa kwenye ukanda wa Afrika Mashariki.Ametoa kauli hiyo leo mchana (Jumamosi, Agosti 30, 2014) wakati alipokutana na Naibu Waziri wa Mambo ya Nje wa Japan, Bw. Hirotaka Ishihara na wafanyabiashara kutoka Japan kwenye ukumbi wa mikutano wa Ofisi ya Waziri Mkuu. Bw. Ishihara anaongoza ujumbe wa wafanyabiashara 70 kutoka makampuni makubwa 14 ya Japan.Akizungumza na Bw. Ishihara na baadhi ya wafanyabiashara waliohudhuria mkutano huo, Waziri Mkuu alisema ni ukweli usiopingika kwamba Japan ni nchi yenye uchumi imara na kwamba licha ya kuwepo kwa mikutano ya TICAD ambayo hutoa fursa kwa Japan kushirikiana na nchi za kiafrika, bado kuna haja ya wao kuelekeza macho yao Afrika kipekee.

Wanawake wataka umuhimu wa uwepo wa masuala ya jinsia katika Katiba



Mwenyekiti wa Umoja wa Wabunge Wanawake Tanzania (TWPG), Mhe. Anna Abdallah akifungua Semina iliyoandaliwa na Umoja huo kwa kushirikiana na Mtandao wa Wanawake na Katiba kwaajili ya Wajumbe wa Bunge Maalum kuhusu masuala ya Jinsia na Katiba iliyofanyika leo 30 Agosti, 2014 kwenye Ukumbi wa Bunge wa Pius Msekwa Mjini Dodoma.
Katibu wa Umoja wa Wanawake Wabunge Tanzania (TWPG), Mhe. Angellah Kairuki (MB) akizungumzia masuala mbalimbali ya kijinsia katika Semina iliyoandaliwa na Umoja huo kwa kushirikiana na Mtandao wa Wanawake na Katiba kwaajili ya Wajumbe wa Bunge Maalum kuhusu masuala ya Jinsia na Katiba iliyofanyika leo 30 Agosti, 2014 kwenye Ukumbi wa Bunge wa Pius Msekwa Mjini Dodoma.

PINDA AKUTANA NA VIONGOZI WA TAASISI YA UTEPE MWEUPE




PG4A3948Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akizungumza na Viongozi wa Taasisi ya Utepe Mweupe(White Ribbon) Ofisini kwake jijini Dar es salaam August 30, 2014. Kutoka kushoto ni Lalia Carasciuc, Rose Mlay, Craig Ferta na Lydia Kamwanza. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)

MWANAAFA MWINZAGO AIBUKA KINARA WA SHINDANO LA TANZANIA MOVIE TALENTS (TMT) 2014 NA KUONDOKA NA KITITA CHA SHILINGI MILIONI 50 ZA KITANZANIA

Mwenyekiti wa Makampuni ya Proin, Bw Johnson Lukaza akitoa neno kwa wadau waliojitokeza kushuhudia fainali ya Shindano la Tanzania Movie Talents (TMT) lililokuwa pia likirushwa live kupitia Kituo Cha Runinga cha ITV
Mwanaafa Mwinzago (katikati) akishangilia Mara baada ya kutangazwa Mshindi wa Kitita Cha Milioni 50 za Kitanzania katika Fainali ya Kumsaka Mshindi wa Shindano la Tanzania Movie Talents (TMT) 2014 lililofanyika usiku wa kuamkia leo katika Ukumbi wa Mlimani City na Kuhudhuriwa na Mamia ya Watanzania.
Mwanaafa Mwinzago (katikati) akiwa katika picha ya Pamoja na wazazi wake na timu ya wafanyakazi wa TMT na washiriki wenzie mara baada ya kukabidhiwa mfano wa Hundi ya Shilingi Milioni 50 za Kitanzania Mara baada ya Kuwabwaga Washiriki wenzie tisa na Kuibuka Mshindi wa Kitita Cha Milioni 50 za Kitanzania katika Fainali ya Kusaka Vipaji Vya Kuigiza Nchini lijulikanalo kama Tanzania Movie Talents (TMT) ambalo limefikia Ukingoni Jana Katika Ukumbi wa Mlimani City.

KIJANA APIGWA HADI KUFA BAADA YA KUIBA SIMU MBEYA



MASIKINI MGUNDUZI WA TANZANITE MZEE NGOMA ANAZIDI KUTESEKA PAMOJA NA KUGUNDUA MADINI YENYE THAMANI KUBWA KWA TAIFA!!


Jumanne Ngoma: Mgunduzi wa tanzanite anayetaabika
- Pia amegundua madini ya jasi yanayotengeneza saruji 

- Apigania kupata sehemu ya mauzo yake bila mafanikio 
- Mkubwa serikalini alimpora sarafi yake Soko la Dunia 
- Ahoji iweje Williamson alipwe kwa kugundua almasi?

POLISI AMGONGA MTOTO, AKIMBIA, ATELEKEZA GARI HUKO MOROGORO



Mtoto Zahara Almeda aliyegongwa na polisi huyo.

MOROGORO. Polisi mmoja ambaye hakufahamika jina lake mara moja, aliyekuwa akiendesha gari kwa mwendo wa kasi, Jumapili iliyopita alimgonga mtoto wa kike, Zahara Almeda katika barabara ya Mji Mpya.

KISA CHA KUTISHA CHA DADA HUYU NA SAKATA LA MADAWA YA KULEVYA


Msichana anayetambulika kwa jina moja la Mary (23) anayedai kuchoshwa na kazi ya kubebeshwa madawa ya kulevya.
  Msichana aliyejitambulisha kwa jina moja la Mary (23), mkazi wa Dar ambaye ni mwenyeji wa Nyegezi, Mwanza, ameangua kilio na kusema; ‘nabebeshwa madawa ya kulevya (unga), nalipwa kiduchu hadi nimechoka’.Awali, gazeti hili lilitonywa na vyanzo vyake juu ya kuwepo kwa ishu hiyo maeneo ya Manzese, Dar ambapo uchunguzi ulifanyika na kumnasa binti huyo ambaye alifunguka kila kitu.

PASTOR MYAMBA APATA AJALI MBAYA YA GARI


Taswira baada ya ajali hiyo.

STAA wa filamu za Kibongo, anayepatia zaidi kuigiza kama Mchungaji, Emmanuel Myamba ‘Pastor Myamba’ amepata ajali baada ya gari lake aina ya Toyota Creasta kugongwa na gari lingine leo mchana katikati ya Boko na Bunju jijini Dar es Salaam.

MWENYEKITI WA CHADEMA MKOA WA TABORA AJIUZULU RASMI, ADAI KATIBA INAKIUKWA NA VIONGOZI WA JUU.


Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo Chadema mkoa wa Tabora Bw.Kansa Mbaruku na Mwenyekiti wa kamati ya Sheria na haki za binadamu kanda ya magharibi ambaye pia ni Mwanasheria mkongwe Bw.Mussa Kwikima wametangaza kujiuzulu rasmi leo hii mbele ya waandishi wa habari kufuatia madai ya kuendelea kukiukwa kwa maadili ya viongozi kuanzia ngazi ya juu ambao wamekuwa wakivunja katiba kwa maslahi yao binafsi.

RAIS KIKWETE AWEKA JIWE LA MSINGI UJENZI WA BARABARA YA MBANDE-KONGWA 16.5KM





Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete akiwa na Waziri wa Ujenzi Dkt. John Pombe Magufuli, Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Dkt. Rehema Nchimbi, Mbunge wa Kongwa ambaye pia ni Naibu Spika Job Ndugai, Makamu Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Miundombinu Profesa Juma Kapuya pamoja na Katibu Mkuu wa Wizara ya Ujenzi Mhandisi Mussa Iyombe, akikata utepe kuashiria uzinduzi rasmi wa barabara ya Mbande-Kongwa 16.5Km.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete wakwanza kushoto akiwa na Waziri wa Ujenzi Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli, Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Dkt. Rehema Nchimbi pamoja na Mbunge wa Kongwa ambaye pia ni Naibu Spika Job Ndugai wakifurahia mara baada ya Rais kuweka jiwe la Msingi Ujenzi wa Barabara ya Mbande-Kongwa 16.5Km .

XABI ALONSO AJIUNGA RASMI NA BAYERN MUNICH



Photo: Xabi Alonso rasmi amejiunga na Bayern Munich

MCHUNGAJI AFIKISHWA MAHAKAMANI KWA KUISHI NA MKE WA MUUMINI WAKE



Pichani ni Mchungaji, Israel Mwakifuna, wa Kanisa la Jeshi la Bwana(JB)lililopo Nzovwe jijini Mbeya 

KATIKA hali isiyokuwa ya kawaida, ambapo wananchi wengi wanaamini Mchungaji ni sehemu ya kukimbilia kueleza matatizo yao hususani migogoro ya kindoa, hali imekuwa tofauti jijini Mbeya.

KIFAA CHA KUCHUNGUZIA UGONJWA WA EBOLA CHAWEKWA AIR PORT ZANZIBAR


Mkuu wa kitengo cha kufuatilia mwenendo wa Maradhi Zanzibar Dkt Salma Masauni akionesha Kifaa “THERMAL SCANNER” kwa Wafanyakazi wa Kituo cha Afya cha Uwanja wa ndege wa Zanzibar. Kifaa hicho kitatumika kusaidia kuwabaini Wagonjwa wa EBOLA watakao ingia nchini kutoka mataifa mengine.
Mkuu wa kitengo cha kufuatilia mwenendo wa Maradhi Zanzibar Dkt Salma Masauni na Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Uhamiaji Zanzibar wakionesha baadhi ya Vifaa Vitalavyotumika kuwachunguza Wagonjwa wa EBOLA watakao ingia nchini kutoka mataifa mengine.

ALIYEKUWA MKURUGENZI WA TBS BWANA CHARLES IKEREGE AHUKUMIWA KWENDA JELA


Mahakama ya hakimu mkazi Kisutu Dar es Salaam, imemhukumu kwenda jela miaka Mitatu aliyekuwa mkurugenzi wa TBS Bwana Charles Ikerege baada ya kukutwa na hatia katika makosa yaliyokuwa yakimkabili, ikiwa ni pamoja na matumizi mabaya ya Ofisi

OKWI AJIUNGA NA SIMBA SC


Msimbazi ni nyumbani; Okwi akiwa na jezi ya Simba SC baada ya kurejea timu yake ya zamani leo

Na Mahmoud Zubeiry, DAR ES SALAAM
STAILI ile ile waliyotumia Yanga SC kumpata mshambuliaji Emmanuel Arnold Okwi ndiyo ambayo klabu yake ya zamani, Simba SC inaitumia kumrejesha kundini Mganda huyo.

Akizungumza na Waandishi wa Habari jioni hii mjini Dar es Salaam, Okwi amesema kwamba amesaini Simba SC mkataba huru wa muda, baada ya Yanga SC kumpa barua ya kusitisha mkataba naye jana pamoja na kumshitaki Shirikisho la Soka Tanzania (TFF).

RAIS KIKWETE KATIKA SHEREHE ZA UZINDUZI WA PROGRAMU YA UIMARISHAJI WA MIPAKA YA KIMATAIFA MKOANI KAGERA


Rais Jakaya Mrisho Kikwete akisalimiana na Rais Pierre Nkurunzinza wa Burundi alipowasili eneo la mpaka kati ya Tanzania na Burundi la Mugikomero wilayani Ngara mkoani Kagera kwa upande wa Tanzania na eneo la Nteritare kwa upande wa Burundi wakati wa sherehe za uzinduzi wa programu ya uimarishaji wa mipaka ya kimataifa Jumatano Agosti 27, 2014.

Viongozi, wanaharakati wataka Katiba Mpya Imtambue mtoto na haki zake


Mwenyekiti wa Mtandao wa Mashirika yanayofanya kazi na Watoto Tanzania ambaye pia ni Mratibu Miradi, Kituo cha Watoto wa Mtaani cha Dogodogo Kigogo (Dogodogo Centre Street Children Trust), Sabas Masawe. 
Mwenyekiti wa Mtandao wa Mashirika yanayofanya kazi na Watoto Tanzania ambaye pia ni Mratibu Miradi, Kituo cha Watoto wa Mtaani cha Dogodogo Kigogo (Dogodogo Centre Street Children Trust), Sabas Masawe.
MCHAKATO wa kujadili na kuandika Katiba Mpya unaendelea bungeni mjini Dodoma, licha ya kuwepo kwa mvutano na mgawanyiko wa makundi ya wabunge wa bunge maalumu wanaojadili Rasimu ya Pili iliyowasilishwa kwao. Wakati hayo yakiendelea viongozi, wanaharakati na wadau wa watoto wanapendekeza masuala ya haki za msingi za watoto yatambulike vizuri katika katiba ijayo.

Liverpool kumenyana na Madrid Uefa


Kocha wa Liverpool Brendan Rodgers


Washindi mara tano wa kombe la klabu bingwa barani ulaya Liverpool watakutana mabingwa watetezi wa kombe hilo Real Madrid.
Liverpool ikiwa imerejea tena kwenye michuano hiyo baada ya kutokuwepo kwa kipindi cha miaka mitano, pia wako kwenye kundi moja na Basel na Ludogorets ya Bulgaria.

MTOTO ABAKWA NA KUUAWA KINYAMA HUKO SHINYANGA WAZIKWA

 

VIONGOZI WA TAKUKURU WAKUTANA KILIMANJARO .


Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro Leonidas Gama akitoa hotuba wakati wa ufunguzi wa mkutano mkuu wa mwaka wa viongozi wa TAKUKURU unaofanyika katika ukumbi wa Kuringe.
Mkurugenzi mkuu wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) Dk Edward Hosea akizummza wakati wa Mkutano wa mkuu wa mwaka wa viongozi wa TAKUKURU .

DKT. FRANCIS MICHAEL ATOA UFAFANUZI KUHUSU SUALA LA UTUNGAJI WA KATIBA


Na Magreth Kinabo, Dodoma
26/08/2014.
 
 Mjumbe wa Bunge Maalum la Katiba, ambaye ni Mwenyekiti wa Kamati Namba  Tatu  ya Bunge hilo, Dkt. Francis  Michael  ametoa ufafanuzi kuhusu suala la utungaji wa Katiba ambalo hufanyika kwa mifumo miwili, na kuwataka wananchi wasipotoshwe na mfumo unaotumika.
 
 Kauli hiyo imetolewa leo na Mwenyekiti huyo, ambaye pia ni mtaalam wa sheria  wakati akizungumza katika kipindi cha Jambo kinachorushwa na  Shirika la Utangazaji Tanzania (TBC).
 
Akifafanua kukuhusu mifumo hiyo, amema kuwa kuna mfumo wa kwanza ,ambao hutumia Tume kama ilivyokuwa Tume ya Jaji Joseph Warioba yenye watu  ambayo ilikuwa na kazi  ya kukusanya na kuratibu maoni ya wananchi na kutengeneza  Rasimu ya Katiba   Mpya , baadaye  Bunge Maalum la Katiba linapitia maoni ya Rasimu hiyo, ambapo kwa mujibu wa Sheria ya Mabadiliko ya Katiba ya mwaka 2014 linaweza kubadilisha na kuongeza kwa ajili ya kuiboresha.
 
“Katika  mfumo huu lazima Bunge liwepo kwa ajili ya kuiboresha kabla ya kwenda kupigiwa kura na wananchi,” alisema Dkt. Michael .

JUKATA WAMBEBESHA LAWAMA SITTA, WASEMA KATIBA MPYA NI NDOTO KUPATIKANA

 Kaimu mwenyekiti wa Uukwaa la Katiba Tanzania Hebron Mwakagenda akizungumza na wanandishi wa habari leo Agosti 27, 2014 juu ya mwenendo wa bunge la katiba.
Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam.
Wakati mchakato wa katiba Tanzania ukiwa ni kama kitendawili kisicho na majibu sahihi kutokana na mchakato huo kuvurugika na kukosa mwelekeo, nao Jukwaa la Katiba Tanzania (JUKATA) wazidi kumtupia lawama zote za kuvurugika bunge hilo mwenyekiti wa bunge hilo mheshimiwa Samweli Sitta na kudai kuwa ndiye aneyeuvuruga mchakato huo baada ya kugeuza Bunge hilo kama kikao cha Chama cha Mapinduzi (CCM).

Taarifa Kwa Umma Kutoka IKULU:Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete ameupa wiki moja uongozi wa Halmashauri ya Wilaya ya Kilosa, Mkoa wa Morogoro, kuwapatia viwanja vya kujenga nyumba wahanga wa mafuriko ya kiasi cha miaka minne iliyopita mjini Kilosa.



Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete ameupa wiki moja uongozi wa Halmashauri ya Wilaya ya Kilosa, Mkoa wa Morogoro,  kuwapatia viwanja vya kujenga nyumba wahanga wa mafuriko ya kiasi cha miaka minne iliyopita mjini Kilosa.



Heri Siku ya Kuzaliwa Waziri Mkuu Mstaafu na Mbunge wa Jimbo la Monduli,Mh. Edward Ngoyai Lowassa


Agosti 26 ni siku ya kuzaliwa ya Waziri Mkuu Mstaafu na Mbunge wa Jimbo la Monduli,Mh. Edward Ngoyai Lowassa aliezaliwa tarehe kama ya leo miaka 61 iliyopita.Mh. Lowassa anayo furaha kubwa kuisherehekea siku hii muhimu kwake na kwa familia kwa ujumla. NDGSHILATU BLOG na timu yake inamtakiwa Heri ya siku ya kuzaliwa kwake.
Mh. Lowassa akiwa shambani kwake wakati alipotembelea kuangalia maendeleo ya mifugo.

SERIKALI YAPOKEA MAGARI NA PIKIPIKI KUKABILIANA NA UGONJWA WA KIFUA KIKUU NA UKOMA NCHINI





Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii, Dkt. Seif Rashidi (kulia) akipokea ufunguo wa moja kati ya magari kutoka kwa mwakilishi wa shirika la GLRA nchini Burchard Rwamtoga (kushoto) ikiwa ni ishara ya kukabidhi msaada wa gari 4 na pikipiki 20 vyenye thamani ya Tsh. Milioni 261 jijini Dar es salaam.
Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii, Dkt. Seif Rashidi akiwasha moja kati ya magari manne  aliyoyapokea kutoka kwa mwakilishi wa shirika la GLRA la Ujerumani nchini Burchard Rwamtoga jijini Dar es salaam.

Diamond na Dabo watajwa kuwania tuzo za 'IRAWMA', Marekani



Wasanii wa Tanzania, Diamond Platinumz na Dabo (wa Dancehall) wametajwa kuwania tuzo za IRAMWA (International Reggae and World Music Awards), Marekani.
Wimbo wa MdogoMdogo wa Diamond umemuwezesha kutajwa kuwania tuzo hizo katika kipengele cha The Best African Song/Entertainer akichuana na Davido (Aye), Awilo Longomba (Bendeke), Willy Paul Msafi (Tam Tam), Eddy Kenzo (Sittya Loss), na Bracket (Mama Afrika).

Nina Mimba ya Mbasha sio Gwajima -Flora Mbasha



Muimbaji wa nyimbo za Injili Tanzania ambae pia ni Mke wa Emmanuel Mbasha amefunguka na kusema kuwa hana mahusiano yoyote ya kimapenzi na na Mchungaji wa Kanisa la kanisa la Ufufuo na Uzima Josephat Gwajima...
Flora amesema hayo leo alipokuwa akichat Live kupitia ukurasa wa Facebook wa EATV katika kipengele cha Kikaangoni Live kinachofanyika kila siku ya Jumatano kuanzia saa Sita kamili.

Flora amesema kuwa hawezi kuwa na mahusiano ya kimapenzi na mtu ambae ni ndugu yake hivyo Mchungaji Gwajima ni mjomba wake na si mpenzi wake kama ambavyo watu wamekuwa wakizusha kwa lengo la kumchafua na kumshushia hadhi.

Zitto Kabwe Afunguka kuhusu Uhusiano wake wa Kimapenzi na Loveness Diva wa Clouds Fm


Kwa mara ya kwanza Mbunge wa Kigoma Kaskazini, Zitto Zuberi Kabwe ameibuka na kuzungumzia uhusiano wake na mtangazaji wa Clouds FM, Loveness Malinzi ‘Diva’ na kufuta uvumi mzito uliokuwa ukizagaa kuwa wawili hao ni wapenzi.

Zitto alifunguka hayo juzi kupitia kipindi cha Mkasi kinachorushwa na Televesheni ya East Africa ambapo alikanusha kuwa hana uhusiano wowote wa mapenzi licha ya kudaiwa kutungiwa wimbo na mtangazaji huyo kama ishara ya penzi lao.“Mh! Kama yeye amenitungia wimbo sijui lakini mimi sina uhusiano naye wowote wa kimapenzi,” alisema Zitto.
Katika mahojiano hayo, mheshimiwa huyo alifungukia skendo nyingine inayomhusisha kutembea na staa wa Bongo Fleva, Mwasiti Almasi na kudai hakuna ukweli wowote juu ya ishu hiyo.

Alisema anaumia zaidi kusikia watu wanavyomhusisha kutembea na Mwasiti kupitia mitandao ya kijamii wakati hakuna ukweli wowote ambapo msanii huyo wanaheshimiana na kufanya naye kazi kwa karibu ili kumsaidia katika harakati zake za muziki.

WAZIRI CHIKAWE AKUTANA NA MWANAHARAKATI WA KIMATAIFA WA HAKI ZA WANAWAKE NA WATOTO, GRACA MACHEL JIJINI DAR LEO



Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mathias Chikawe (Kushoto) akizungumza na Mwanaharakati wa Kimataifa wa haki za wanawake na watoto, Graca Machel katika  Hoteli ya Serena jijini Dar es Salaam leo.Waziri Chikawe alimueleza Mama Machel, juhudi zake za kuingiza katika Katiba Mpya kifungu cha kuzuia mtoto wa chini ya miaka 18 asioe wala asiolewe.
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mathias Chikawe (kulia) akiagana na Mwanaharakati wa Kimataifa wa haki za wanawake na watoto, Graca Machel baada ya kikao chao kifupi kilichofanyika katika Hoteli ya Serena jijini Dar es Salaam leo. Waziri Chikawe alimueleza Mama Machel, juhudi zake za kuingiza katika Katiba Mpya kifungu cha kuzuia mtoto wa chini ya miaka 18 asioe wala asiolewe. 

BLOG RAFIKI

© Copyright EMMANUEL SHILATU - BREAKING NEWS BLOG
Back To Top